WATANZANIA WATAKIWA KUMUOMBE RAIS SAMIA SULUHU HASSAN

Na. Mwandishi Wetu, DODOMA

WATANZANIA wameshauriwa kufanya dua na sala ya kumwombea Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ili aweze kukamilisha kwa wakati miradi mikubwa iliyoanzishwa na kuachwa na aliyekuwa Rais, Dkt. John Magufuli ambayo imelenga kuwafanikisha watanzania kuwa na maendeleo.



Rai hiyo imetolewa Mhubiri wa kimataifa Mchungaji Nicodemus Mganga wa kanisa la Evangelists Assemblies of God (TZ) Bagamoyo alipokuwa akizungumza na waumini wa kanisa la Nazareth Temple Ipagala (EAGT) Dodoma.

Mchungaji Mganga alisema kuwa watanzania wana jukumu kubwa la kumwelekezea Mungu maombi kwa ajili ya Rais Samia Suluhu ili aweze kukamilisha miradi iliyopo ambayo tuliyoachiwa na aliyekuwa Rais wetu kwa ajili ya maendeleo ya wananchi wake.

Alisema kuwa Rais Magufuli ametuachia mambo mengi ambayo yamelenga kuifanya nchi ya Tanzania kukua zaidi kichumi,hivyo tuna kila sababu ya kuhakikisha tunamhezi pia kwa kumuombea kutokana na mzigo mkubwa aliokuwanao kwa ajili ya wananchi wake.

Hata hivyo watanzania wanatakiwa kuwa na imani kubwa na Rais Samia Suluhu ukizingatia kuwa yeye ndiye aliyekuwa makamu wake kwa maana hiyo yale yote aliyokuwa akifanya Rais Magufuli kwa upande wake atafanikisha tena kwa spidi kubwa.

Awali akizungumza na waumini Askofu mstaafu, Dkt. Evance Chande amewataka watanzania kufanya kazi kwa juhudi kubwa,ikiwemo na ulipaji kodi ili Tanzania ifanikiwe kwenye malengo yake ya kuwafikishia watanzania maendeleo yao.

Dkt. Chande alisema kuwa hakuna sababu ya kukaa bila kufanya kazi na ukwepaji wa kodi,kinachotakiwa kuiunga serikali ambayo imekuwa mstali wa mbelel katika kuhakikisha watu wake wanaondokana na umasikini usiokuwa na tija.

Askofu huyo mstaafu alisema watanzania wakishiriki kwa uaminifu katika kufanya kazi na kulipa kodi, serikali iliyopo chini ya Rais Samia Suluhu itakuwa namaendeleo ambayo yatakayoenda kwa haraka na wepesi kwa kuwafikia watu bila kujali itikadi yoyote.

 

MWISHO

 

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.