WATANZANIA WATAKIWA KUENDELEA KUMUAMINI MUNGU

Na. Mwandishi Wetu, DODOMA

 

Wito umetolewa kwa Watanzania kuendelea kumwamini Mungu aliyewaumba wanadamu wote hasa katika kipindi hiki ambacho Taifa linapitia katika msiba mkubwa na mzito wa kuondokewa na Kiongozi Mkuu wa Taifa Hayati Dkt. John Pombe Magufuli.

Wito huo umetolewa na Katekista Yonah Kusaja wa Kanisa la Aglikana Parish ya Mtakatifu, Stephano-Kikombo Jijini Dodoma wakati wa mahojiano maalumu na mwandishi wetu ambapo amesema kuwa,Mungu alitupa Kiongozi huyo kama zawadi, hivyo ni yeye pia ndiye aliyeamua kutunyang’anya zawadi hio.

 

Ametoa wito kwa Watanzania kuyaishi mambo mema yaliyo asisiwa na Hayati Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, sanjari na kuendelea kumtegemea Mungu katika kila jambo kama ambavyo Marehemu alikuwa akisisitiza enzi za uhai wake.

 

Hata hivyo Katekista Kusaja amemuomba Rais wa sasa Mhe. Samia Suluhu Hasani kwa nafasi yake kuyaendeleza mambo mema aliyoyaanzisha mtangulizi wake na kuyakamilisha kwa wakati.

 

Kwa upande wake Mchungaji Paniel Nnko wa Kanisa la Christian Center Miyuji Jijini Dodoma amesema kuwa, Taifa limempoteza Kiongozi mzalendo ambaye aliyatoa maisha yake yote kuhakikisha anaongoza mapambano dhidi ya rushwa, ufisadi na uzembe kazini.

 

Aidha, Mchungaji Nnko amewamba Wakristo na Watanzania wote kwa ujumla kuliombea Taifa katika kipindi hiki cha maombolezo liwe na amani na utulivu, huku nae akimuomba Rais Samia na Viongozi wote serikalini kuwatumika vyema Watanzania kwa kutanguliza maslahi ya Taifa kwanza, kutenda haki na kuweka uzalendo mbele.

 

 

MWISHO

 

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.