MAELEZO MAFUPI YANAYOMUHUSU MAKAMU WA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGAMO WA TANZANIA DR. PHILIP ISIDORY MPANGO

 



Dk Philip Mpango ametokea  katika  nafasi ya  Waziri wa Fedha na Mipango katika Serikali ya Awamu ya Tano, ameteuliwa katika baraza la mwanzo la mawaziri la Rais John Magufuli. Alikuwa  ni  mbunge katika  jimbo  la Buhigwe mkoani  Kigoma ambapo Katika  uchaguzi uliopita  wa Octoba 2020 Dkt Mpango  alipita  bila  kupingwa.

Mpango ni mzaliwa wa Kigoma, baba yake ni marehemu Isidori Nzabhayanga Mpango, ambaye alizaliwa Kijiji cha Kasumo, Wilaya ya Kasulu. Dk Mpango alizaliwa hapo hapo Kasumo na ni kaka mdogo wa Askofu mstaafu wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Tanganyika Magharibi – Kasulu  mkoani Kigoma, Dk Gerard Mpango.Dk Mpango ni mchumi mwenye shahada ya uzamivu ya uchumi.

Kuanzia miaka ya 1990 hadi 2000, alifanya kazi akiwa mhadhiri mwandamizi wa uchumi katika kitivo cha Biashara (sasa Shule ya Biashara) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

Alikuwa akifundisha “Microeconomics”, “Macroeconomics” (kwa mwaka wa pili) na “Public Finance” kwa mwaka wa tatu na kozi za uzamili ambayo ni  Uchumi mdogo, Uchumi mkubwa na masuala ya Fedha za umma.

Amewahi kuwa Mchumi Mwandamizi wa Benki ya Dunia, Mkuu wa Kamati ya kumshauri Rais Jakaya Kikwete wakati huo kuhusu masuala ya uchumi, Katibu binafsi wa Rais anayeshughulikia masuala ya uchumi, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Uchumi, kabla ya kuhamishiwa Tume ya Mipango, Ofisi ya Rais. Nyadhifa hizi zote amezishika wakati wa utawala wa Kikwete.

JPM alipoingia madarakani alimteua kuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na baada ya siku chache akateuliwa kuwa Waziri wa Fedha na Mipango.

Dk Mpango ni kiongozi mwenye msimamo thabiti. Baadhi ya watendaji ambao wamewahi kufanya kazi chini yake kwenye ofisi ya Rais wanamuelezea kama mtu anayetaka waliomzunguka wazungumze kwa takwimu na ushahidi hasa katika masuala ya uchumi. Msimamo huo pia aliuonyesha alipokuwa mtaalamu wa Benki ya Dunia. Hakuwa mwoga kuieleza ukweli Serikali pale ambako ilikuwa haifanyi vizuri.

Ni kiongozi mwenye dira na maono mapana, ni mtendaji anayeweza kusimamia jambo alilokabidhiwa na likafanikiwa. Alipoteuliwa kuwa Kaimu Kamishna Mkuu wa TRA, ndani ya mwezi mmoja ukusanyaji wa mapato wa taasisi hiyo ulivunja rekodi. Kwa mara ya kwanza TRA ilikusanya zaidi ya Sh1.4 trilioni kwa mkupuo. Rais JPM alijitokeza na kumpongeza kwa hatua hiyo na muda mfupi baadaye akamkabidhi Wizara ya Fedha.

Philip Mpango  alizaliwa Julai 14, 1957  ni  alikuwa  Waziri wa Fedha  wa Tanzania  akiwa ofisini tangu Machi 2015. Mpango hapo awali alishikilia nafasi kama kaimu kamishna mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), [3] katibu mtendaji  katika  Ofisi  ya Rais (Tume ya Mipango), naibu katibu mkuu wa Wizara ya Fedha na Uchumi, msaidizi binafsi wa rais (masuala ya uchumi), mkuu wa Kitengo cha Ushauri wa Kiuchumi wa Rais, na kama mchumi mwandamizi wa Benki ya Dunia.

Mara  baada  ya  kuteuliwa  jana  machi 30,2021  katika Mkutano  wa  tatu  kikao cha  kwanza  cha  Bunge la Jamhuri  ya Muungano  wa Tanzania  kuwa Makamu   wa  Rais  jimbo  la BUHIGWE    limetangazwa  na spika  wa Bunge  hulio  Job Ndugai   kuwa  lipo  wazi.

Mwisho.

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.