Kusaya-vyuo vya mafunzo ya kilimo ni kitovu cha kuzalisha wataalamu wa kilimo

 


Na Jackline Kuwanda,Dodoma.

Serikali kupitia Wizara ya Kilimo imegawa vifaa vya Tehama vyenye thamani ya shilingi Milioni mia mbili arobaini na mbili ,elfu sitini na sita,mia tisa hamsini na tisa na senti thelathini (242,66,959.30)  kwa vyuo 29 vya kilimo.

Akizungumza wakati wa kugawa vifaa hivyo Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Gelard Kusaya amesema ili kufanikisha mafunzo kwa njia ya mtandao yanatolewa ni muhimu kuwa na vifaa vya kisasa na  vyenye uwezo .

Aidha Kusaya amesema vyuo vya mafunzo ya  kilimo ni kitovu  cha kuzalisha wataalamu wa kilimo kwa lengo la kutoa maarifa na ujuzi kwa wakulima ili waweze kuzalisha kwa tija na kujiongezea kipato.

Kwa upande wake Makamu Mkuu wa Chuo cha Karuc Afra Rwechungura ameishukuru Serikali kupitia Wizara ya kilimo kwa kutambua mchango wa vyuo visivyo vya kiserikali katika kufundisha na kutoa wataalamu katika kilimo .

Naye Mkuu wa Chuo cha Mlingano Mhandisi Samson Cheyo amesema kupitia vifaa hivyo vitasaidia kwenda kuboresha utoaji wa mafunzo kwa wanafunzi kwa njia za kisasa ili kutoa wataalamu wanaoweza kuajirika hapa nchini.

Mwisho.

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.