HAYATI DKT MAGUFULI KUENDELEA KUKUMBUKWA KWA HAYA..

 


DAR ES SALAAM

Mkurugenzi wa Taasisi ya Alhikma inayoandaa mashindano ya Qur-an Afrika Sheikh Nurdin Kishk amesema taasisi hiyo itamkumbuka Hayati Magufuli kwa mchango wake ikiwemo kutoa eneo lenye ukubwa wa hekari moja na nusu kwa shirika hilo kwa ajili ya kujenga eneo kubwa la ibada

Hayati Dkt John Pombe Magufuli atakumbukwa kwa mengi hasa katika mchago wake wa kuhakikisha taasisi za kidini zinafanya kazi zake kwa uhuru bila wasiwasi na wakati fulani ilishuhudiwa akiongoza harambee iliyolenga kujenga msikiti jijini Dodoma pia aliwahi kutoa eneo lenye ukubwa wa hekari moja na nusu kwa taasisi ya Alhkma kwa ajili ya kuendeleza kutoa mafunzo ya kumjua Mwenyezi Mungu

Katika hatua nyingine Taasisi hiyo imetambulisha mashindano ya 21 ya Qur-an tukufu Afrika yatakayofanyika April 25 mwaka huu ambapo siku hiyo pia itatumika kusoma dua Maalum ya kuliombea taifa juu masuala mbalimbali ikiwemo kuliombea Taifa juu liepushwe na magonjwa mbali mbali

Sheikh Nurdin Kishk pia amewasihi watanzania kumuunga mkono Rais mpya wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ili aweze kuendeleza kazi iliyoachwa na hayati Dkt John Pombe Magufuli.

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.