Wizara ya maji yaahidi sh.milioni 309 mradi wa maji Ilolo-Bulongwa Jimbo la Makete

Na. Joyce Kasiki, MAKETE

 

KATIBU Mkuu wa Wizara ya Maji, Mhandisi Anthony Sanga ametembelea kwenye milima ya Kisajanilo wilayani Makete kwa ajili ya kufuatilia chanzo cha mradi wa Maji ya Ilolo-Bulongwa na kuahidi kutoa sh. milioni 309 kwa ajili ya kuukamilisha mradi huo ili uanze kutoa maji.

 


Katibu Mkuu huyo akiwa ameongozana na mbunge wa Makete Festo Sanga katika mradi huo ulioibuliwa na wananchi mwaka 2018 na ametanguliza kiasi cha shilingi milioni 100 na kutoa miezi miwili kwa Mamlaka ya Maji Vijijini (RUWASA) mradi huo uanze kufanya kazi.

Akizungumza mara baada ya kutembelea chanzo hicho cha maji Mhandisi Sanga amewapongeza wananchi kwa kuibua chanzo hicho cha maji lakini pia amempongeza Mbunhe wa Jimbo hilo ambaye amekuwa akifuatilia suala hilo mara kwa mara Wizarani ili Serikali iunge mkono juhudi hizo za wananchi na waweze kupata huduma ya maji safi na salama.

"Rais anawapongeza kwa jitihada za kuibua miradi na kutumia nguvu zenu kuianzisha,mmeanzisha mradi huu

miaka miwili imepita, Mbunge amenisumbua sana na nimefanya naye vikao zaidi ya mara tatu juu ya hali ya maji Makete na nimeamua kufika hapa   ili tushughulikie changamoto za maji"alisema Mhandiai Sanga na kuongeza kuwa 

"Serikali ni sikivu na ninawaagiza RUWASA ndani ya siku 60 mradi huu ukamilike, jumanne (kesho kutwa) tutaleta milioni 100 za kuanzia"

Mbali na kutembelea mradi huo pia Katibu Mkuu huyo akiongozana na Mbunge wa Jimbo hilo watatembelea kata ya Lupila, Tandala na Lupalilo kwa ajili ya kuangalia miradi ya maji.

 

MWISHO

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.