Na. Albano Midelo, Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma
WAZIRI
Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa ameiagiza mikoa na Mamlaka zote za serikali za
mitaa kutenga bajeti ya kuyahifadhi maeneo yote ya kihistoria ili kutopoteza
historia yake kwa manufaa ya Taifa.
Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Innocent Bashingwa ambaye alimwakilisha Waziri Mkuu katika tamasha la miaka 114 ya mashujaa wa vita ya Majimaji |
Majaliwa
ametoa agizo hilo katika hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Waziri wa
Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Innocent Bashungwa kwenye kilele cha tamasha
la kumbukizi ya miaka 114 ya vita ya Majimaji lililofanyika kwenye viwanja vya
Makumbusho ya Taifa ya Majimaji mjini Songea.
Waziri
Mkuu pia ameiagiza Wizara ya Maliasili na Utalii kuendelea kuadhimisha
kumbukizi hizo ili ziwe sehemu ya vivutio vya utalii nchini ambazo zinachangia
kuongeza pato la Taifa na kwamba Wizara hiyo kwa kushirikiana na Wizara ya
Habari zihamasishe na kuelimisha jamii fursa za kumiliki maeneo ya malikale.
Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo InnocentBashungwa akiweka ngao kwenye mnara wa mashujaa wa vita vya Majimaji ambapo mashujaa 67 walinyongwa na wajerumani mwaka 19069 |
Akizungumzia
mashujaa wa vita ya Majimaji, Waziri Mkuu ameagiza kumbukumbu zilizopo ndani ya
Makumbusho ya Taifa ya Majimaji zinaendelea kuhifadhiwa ili kujenga uzalendo na
kuleta utaifa kwa kizazi kilichopo na kijacho.
“Mkoa
wa Ruvuma hivi sasa una makumbusho mawili ambayo ni Makumbusho ya Majimaji na
Makumbusho ya Dkt. Hayati Rashid Mfaume Kawawa,Mkoa huu ndiyo kitovu cha kusaidia
wanaharakati wa ukombozi wa Afrika hususan nchi jirani ya Msumbiji’’,alisisitiza
Waziri Mkuu.
Kwa
upande wake Waziri wa Maliasili na Utalii ambaye pia ni Mbunge wa Songea mjini,
Dkt. Damas Ndumbaro akizungumzia
kumbukizi ya miaka 114 tangu kunyongwa mashujaa wa vita Majimaji,amesema
maadhimisho hayo yamelenga kuenzi ushujaa
wa wazee wetu katika harakati za awali za ukombozi dhidi ya wakoloni.
Imanuel Zulu Chifu wa Tano wa kabila la wangoni akizungumza kwenye kumbuzi ya miaka 114 ya vita ya Majimaji |
“Maisha
ya wazee wetu ni fahari yetu kwa sababu wazee hawa walipigania nchi kwa
uzalendo wa hali ya juu,ukombozi wa mwafrika una historia kubwa sana hapa kwa
sababu mapambano yaliyofanyika kwa muda mrefu zaidi dhidi ya mkoloni nchini
Tanzania yalifanyika Songea’’, alisema Dkt. Ndumbaro.
Mwakilishi
wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Christawaja Ntandu ameyataja
malengo ya tamasha la kumbukizi ya mashujaa wa majimaji ambalo hufanyika kila
mwaka kuwa ni kukumbuka na kuwaenzi
mababu zetu ambao walinyongwa Februari 27,1906 na kuzikwa kwenye makaburi
mawili ndani ya makumbusho ya Majimaji.
Hata
hivyo amesema tamasha hilo hutoa fursa kwa wananchi kutunza,kuenzi na
kuendeleza uzalendo,amani na mshikamo ambao umerithiwa kutoka kwa mababu zetu
na kwamba tamasha hilo pi hutumika kuibua na kutangaza vivutio vya utalii
vilivyopo ukanda wa kusini.
Naye
Mkurugenzi wa Makumbusho ya Taifa, Dkt. Noel Lwoga amesema wazee waliopigana
katika vita ya Majimaji miaka 114 iliyopita dhidi ya wakoloni walitoa mchango
mkubwa katika kutetea taifa letu na kwamba vita ya Majimaji imebeba utajiri
mkubwa wa historia ya ukombozi na uhuru wa nchi yetu.
Comments
Post a Comment