Na. Fatuma Malende, CHATO
Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Mhandisi Maryprisca
Mahundi (Mb) ametoa onyo kwa Meneja wa Wakala wa MajiSafi na Usafi wa Mazingira
Vijijini (RUWASA) Chato, Mhandisi Andrew Kilembe kwa kushindwa kutatua kwa wakati
kero ya ubovu wa mita za maji zilizowekwa katika mradi wa maji wa Imalabupina
Inchwankima na kusababisha wananchi wa eneo hilo kukosa maji kwa siku kadhaa.
Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Maryprisca Mahundi (Mb) akikagua miundombinu ya mradi wa maji wa Imalabupina Inchwankima |
Ametoa onyo hilo baada ya kupokea malalamiko toka
kwa wananchi wakati akikagua mradi huo unahohudumia wakazi wa vijiji hivyo.
Amesema wananchi wanakosa huduma ya maji kwa sababu
ya viongozi kufanya kazi kwa mazoea na kushindwa kutatua kero zinazojitokeza
kwa wakati.
“Natoa onyo na naomba fuatilieni hilo tatizo
linalosababisha wananchi wasipate maji kwa wakati maeneo mengine yanatoa maji,
na hakikisheni hizo mita zinazosumbua zinabadilishwa haraka ili kuondoa kero hiyo
na wananchi hawa wapate maji”, amesema Mhandisi Mahundi na kusisitiza kezo zote
ikiwemo matatizo ya umeme yasisubiri viongozi.
Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Maryprisca Mahundi (Mb) akiwa ofisini kwa Mkuu wa Wilaya ya Chato, Eng. Charles Francis Kabeho kabla ya kuanza ziara ya kukagua miradi ya maji katika Wilaya ya Chato |
Aidha, amempongeza Meneja huyo wa RUWASA Chato kwa
kuamua kutumia shilingi milioni 311 kukarabati miundombinu ya mradi wa maji
Kasenga ambao ulichakaa na kuacha kutoa maji kwa muda mrefu.
Katika ziara yake ya kukagua miradi ya maji mkoani
Geita Naibu Waziri alikagua pia mradi wa maji wa Katoro Buseresere ambao
utekelezaji wake unaendele vizuri na mradi huo ukikamilika utahudumia wananchi 20,000
wa kata ya Buseresere, Katoro, Ludete na Nyamigota.
Tenki la maji la mradi wa maji Katoro ambalo ujenzi wake unaendelea viruzi linasimamiwa na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Geita (GEUWASA). |
Comments
Post a Comment