JKT na wizara ya kilimo wasaini mkataba wa maridhiano Na Rhoda Simba, DODOMA

JESHI la kujenga Taifa (JKT) limetia saini mkataba wa maridhiano na Wizara ya Kilimo wenye lengo la kuhakikisha Taifa linapata chakula cha kutosha.

 

Kushoto ni katibu mkuu wizara ya kilimo, Gerald kusaya na kulia ni meja generali Charles mbuge mkuu wa Jshi la Kujenga Taifa

Akizungumza leo Jijini hapa Mkuu wa Jeshi la kujenga Taifa JKT Meja Generali Charles Mbuge amesema mashirikiano hayo yana lengo la kulinufaisha taifa kwani Taifa likiwa na njaa  shughuli za kiuchumi haziwezi kufanyika.

 

 

Aidha Meja Generali Mbuge amesema kilimo ndio uti wa mgongo ambapo kwa Tanzania Kilimo kinahusisha matabaka yote  wenye kipato na wasio na kipato

 

"Makubaliano hayo Kati yaJeshi la kujenga Taifa (JKT) yamekuja wakati muafaka kwani vijana wengi wa Tanzania wamekua wakijitolea kwenye mafunzo hivyo wakiwa ndani ya JKT watapatiwa mafunzo ya Kilimo ambapo na wao wataenda kuitumia vizuri pindi wawapo uraiani.

 

 

Na nakuongeza kusema kuwa "Jeshi ni chombo pekee ndani ya Taifa letu hivyo endapo likitumiwa vizuri litaleta manufaa makubwa katika Taifa"amesema 

 

Hata hivyo amesema JKT imeshaanza shughuli za Kilimo kwa mazao ya kimkakati Katika maeneo mbalimbali ya hapa Nchini.

 

Naye Kanali Hassan Mabena ambae ni Kaimu Mkuu wa utawala  Jeshi la kujenga taifa (JKT )amesema lengo la kuwekeana saini ni kuhakikisha Taifa linajitosheleza kwa chakula na kulipunguzia Taifa mzigo.

 

"Jeshi la kujenga Taifa (JKT) limejiwekezea nguvu kubwa katika vikosi vyake kwani mazao yote ya kimkakati  yanalimwa Katika vikosi hivyo"

 

Aidha amebainisha changamoto wanazokumbana nazo katika Kilimo ni mabadiliko ya tabia nchi, na uhaba wa pembejeo za Kilimo.

 

Naye Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Gerald Kusaya amesema makubaliano hayo yalikua ni ndoto yake ya kila siku kwani yeye ni mfatiliaji mkubwa katika shughuli wanazo fanya  Jeshi la Kujenga Taifa (JKT).

 

kukutana kwao na kutiliana saini ni moja wapo ya Malengo Makubwa kwani JKT shughuli za kilimo wanazo fanya zinajulikana ila wizara ya kilimo ndio vinara.

 

MWISHO

 

 

 

 

 

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.