WIZARA YAELEZA MIKAKATI YA KUMALIZA TATIZO LA SUKARI NCHINI

Na. Beatrice Kimwaga, WIZARA YA KILIMO

Waziri wa kilimo, Prof. Adolf Mkenda amefanya mkutano na waandishi wa habari kuhusiana na hali ya uzalishaji wa sukari hapa nchini.

Picha sukari : Waziri wa kilimo Prof. Adolf Mkenda akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma kuhusiana na uzalishaji na mipango ya kujitosheleza kwa sukari nchini. 
Kulia kwake ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Bw. Gerald Kusaya na kushoto kwake ni Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi wa bodi ya sukari Bi.Mwamini Malemi


Prof. Mkenda amesema kuwa uzalishaji wa sukari hapa nchini umekuwa ukiongezeka katika kipindi cha miaka mitano uzalishaji wa sukari umeongezeka kwa asilimia 78.3 (kutoka tani 295,775 mwaka 2015/2016 hadi tani 377,527 zinatarajia kuzalishwa msimu wa 2020/2021)

Hata hivyo Prof.Mkenda amesema kuwa mafanikio haya ya kuongezeka kwa uzalishaji ni matokeo ya utekelezaji wa sera na mikakati ambayo serikali imeweka kuhakikisha wazalishaji wana mazingira mazuri ya kufanya upanuzi wa mashamba na wakulima kuongeza tija.

Aidha, katika msimu wa mwaka 2020/2021 jumla ya tani 377,527 za sukari zitazalishwa kutoka kwenye viwanda vilivyopo vya Kilombero Sugar Company Ltd, Mtibwa Sugar Estate, Kagera Sugar Ltd, TPC Ltd na Manyara Sugar Ltd. Pia amesema kuwa mahitaji ya sukari kwa ujumla hapa nchini kwa matumizi ya kawaida na viwandani ni tani 655,000 kwa mwaka.

Pof. Mkenda ameendelea kusema kuwa ili kuongeza uzalishaji Serikali imejipanga kuboresha miundombinu ya umwagiliaji kwa wakulima wadogo, viwanda viongeze uwezo wa kuchakata miwa inayozalishwa na kuongeza tija kwa uwepo wa mbegu bora na viuatilifu.

Kutokana na uhaba wa sukari uliopo na miwa ya wakulima kubaki mashambani bila kuvunwa kwa sababu ya ufanisi na uwezo mdogp wa viwanda, serikali imeelekeza Kiwanda cha Kilombero na viwanda vingine kuongeza na kuimarisha uwezo wa uchakataji wa miwa ili kunusuru hasara kubwa wanayoipata wakulima kwa kutovuniwa miwa yao na kupelekwa kuchakatwa viwandani alisema Prof. Mkenda

Serikali haitosita kuchukua hatua ya kuruhusu mwekezaji mwingine kujenga kiwanda cha kati kimoja au viwanda vidogo viwili endapo mwekezaji aliyopo sasa katika bonde la Kilombero atashindwa kufanya upanuzi unaostahili kwa wakati ili miwa ya wakulima wadogo takribani tani 200,000 inayobaki katika bonde la kilombero ipate soko la uhakika.

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.