Na. Beatrice Kimwaga, WIZARA YA KILIMO
Waziri
wa kilimo, Prof. Adolf Mkenda amefanya mkutano na waandishi wa habari kuhusiana
na hali ya uzalishaji wa sukari hapa nchini.
Kulia kwake ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Bw. Gerald Kusaya na kushoto kwake ni Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi wa bodi ya sukari Bi.Mwamini Malemi |
Prof.
Mkenda amesema kuwa uzalishaji wa sukari hapa nchini umekuwa ukiongezeka katika
kipindi cha miaka mitano uzalishaji wa sukari umeongezeka kwa asilimia 78.3
(kutoka tani 295,775 mwaka 2015/2016 hadi tani 377,527 zinatarajia kuzalishwa
msimu wa 2020/2021)
Hata
hivyo Prof.Mkenda amesema kuwa mafanikio haya ya kuongezeka kwa uzalishaji ni
matokeo ya utekelezaji wa sera na mikakati ambayo serikali imeweka kuhakikisha
wazalishaji wana mazingira mazuri ya kufanya upanuzi wa mashamba na wakulima
kuongeza tija.
Aidha,
katika msimu wa mwaka 2020/2021 jumla ya tani 377,527 za sukari zitazalishwa
kutoka kwenye viwanda vilivyopo vya Kilombero Sugar Company Ltd, Mtibwa Sugar
Estate, Kagera Sugar Ltd, TPC Ltd na Manyara Sugar Ltd. Pia amesema kuwa mahitaji
ya sukari kwa ujumla hapa nchini kwa matumizi ya kawaida na viwandani ni tani
655,000 kwa mwaka.
Pof.
Mkenda ameendelea kusema kuwa ili kuongeza uzalishaji Serikali imejipanga
kuboresha miundombinu ya umwagiliaji kwa wakulima wadogo, viwanda viongeze
uwezo wa kuchakata miwa inayozalishwa na kuongeza tija kwa uwepo wa mbegu bora
na viuatilifu.
Kutokana
na uhaba wa sukari uliopo na miwa ya wakulima kubaki mashambani bila kuvunwa
kwa sababu ya ufanisi na uwezo mdogp wa viwanda, serikali imeelekeza Kiwanda
cha Kilombero na viwanda vingine kuongeza na kuimarisha uwezo wa uchakataji wa
miwa ili kunusuru hasara kubwa wanayoipata wakulima kwa kutovuniwa miwa yao na
kupelekwa kuchakatwa viwandani alisema Prof. Mkenda
Serikali
haitosita kuchukua hatua ya kuruhusu mwekezaji mwingine kujenga kiwanda cha
kati kimoja au viwanda vidogo viwili endapo mwekezaji aliyopo sasa katika bonde
la Kilombero atashindwa kufanya upanuzi unaostahili kwa wakati ili miwa ya
wakulima wadogo takribani tani 200,000 inayobaki katika bonde la kilombero
ipate soko la uhakika.
Comments
Post a Comment