Na Saleh Ramadhani
Kaimu Mganga Mkuu Wa Serikali, Dkt. Saitor Laiza amebainisha kuwa Watoto
wenye umri wa chini ya miaka mitano na watu wenye umri wa kati wapo kwenye
hatari kubwa ya kupata maabukizi ya ugonjwa wa kichocho.
Hayo yameelezwa na Kaimu mganga mkuu wa
serikali,
Dkt. Saitor Laiza katika mkutano na wadau wa
afya uliokuwa na lengo la kufahamishana juu ya matokeo ya utafiti ya
ugonjwa wa kichocho uliofanywa na NIMR katika kipindi cha miaka miwili
Kaimu mganga mkuu wa serikali amesema matokeo yanaonyesha kuwa
baadhi ya maeneo hapa nchini bado yanachangamoto ya ugonjwa huo hasa maeneo
yanayozunguka kanda ya ziwa huku idadi kubwa ya Watoto wenye umri
chini ya miaka mitano wakiadhirika zaidi.
"Ugonjwa wa kichocho bado ni
changamoto kubwa katika maeneo ya ziwa victor,ziwa Nyasa na ziwa
Tanganyika,idadi kubwa ya watoto na watu wenye umri wa kati hadi miaka 55
waliopimwa katika Eneo la Ukerewe wameathirika katika sehemu kubwa na Tafiti
kama hizi zinatuamsha sisi watekelezaji wa mifumo ya Afya na Matibabu" amesema.
Aidha, amezielekeza na kuzishauri mamlaka
zinazohusika ikiwemo tamisemi kwakuwa wao wana mamlaka makubwa
kufika katika maeneo yaliyoathirika kuona namna ya kusaidia kuwatibu ilikuokoa
vifo vingi ambavyo vinaweza kutokea.
"Nizishauri Mamlaka husika kama
ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) ambao ndiyo watekelezaji
wakubwa katika maeneo ambayo yanamadhara makubwa hata katika bajeti zetu
tuzipange vizuri ili tuweze kuwaokoa watoto wasiende kuwa na madhara ya muda
mrefu na pia tutaokoa vifo vingi" amesema.
Naye Mkurugenzi wa kuratibu na kukuza
utafiti NIMR na mtafiti kiongozi wa mradi wa tiba, Dkt. Paul Kazyoba ameeleza s kuwa
waliamua kufanya utafiti juu ya ugonjwa huo baada ya kuna haupewi kipaombele
kama magonjwa mengine na kubaini kuwa Watoto chini ya umri wa miaka mitano
wanaathirika Zaidi hasa katika Wilaya
za Nyasa na Ukerewe.
"Katika
mkutano wetu tumeangalia ukubwa wa tatizo la kichocho kwa watoto umri chini ya
miaka mitano,ni moja ya Tafiti ambazo zipo kwenye Mradi wa Tiba na Matokeo yake
yapo Tayari kufanyiwa Kazi ili kuondoa Tatizo la kichocho nchini" Amesema
kazyoba.
MWISHO
Comments
Post a Comment