Na. Albano Midelo, Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma
MKUU
wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme amewaagiza maafisa Tarafa na viongozi wote
ngazi ya Wilaya kusimamia utunzaji wa vyanzo vya maji ili viwe endelevu.
Aliyesimama ni Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme akiongoza kikao cha wadau wa maji mkoani Ruvuma |
Mndeme ametoa agizo hilo wakati anafungua mkutano wa wadau wa sekta ya maji mkoani Ruvuma kilichofanyika kwenye ukumbi wa Manispaa ya Songea.
Mndeme
pia ameagiza wote wanaofanya shughuli za kiuchumi kwenye vyanzo vya maji
kuondolewa na kuchukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria ya mazingira ya mwaka 2004
ya sheria ya RUWASA ya mwaka 2019.
Maagizo
mengine yaliyotolewa na Mkuu wa Mkoa katika kikao hicho ni Halmashauri zote na
sekretarieti ya Mkoa kuwajibika kikamilifu katika kutekeleza na kusimamia
majukumu yote yaliyoorodheshwa kwenye sheria namba tano ya huduma ya maji ya
mwaka 2019.
“Mameneja
wa RUWASA Wilaya kwa kushirikiana na Halmashauri zote zihakikishe kwamba miradi
iliyopo na mingine itakayojengwa inaunda vyombo huru vya watumiaji maji kwa
sheria namba tano ya mwaka 2019 kabla au ifikapo Mei 31,2021’’,alisisitiza
Mndeme.
Mndeme
pia ameagiza katika kikao cha Baraza la madiwani cha kila robo katika
Halmashauri zote iwepo mada ya kudumu ambapo Mameneja wa RUWASA katika wilaya
husika watatoa taarifa kuhusu hali ya upatikanaji na usajili wa vyombo vya
watumiaji maji.
Mkuu
wa Mkoa pia ameagiza RUWASA Wilaya na
Mkoa zishirikiane na Mamlaka ya Majisafi
na Usafi wa mazingira SOUWASA sanjari na ofisi za mabonde ya maji katika
kutafuta vyanzo vya maji na kuandaa mipango ya utunzaji wa vyanzo vya maji.
Baadhi ya wadau wa maji mkoani Ruvuma wakifuatilia kikao cha kilichofanyika ukumbi wa Manispaa ya Songea kikiongozwa na Mkuu na Mkuu wa mkoa wa Ruvuma |
“Naagiza
fedha zitokanazo na mauzo ya maji zikaguliwe na mkaguzi wa ndani wa Halmashauri
ili kujiridhisha namna fedha hizo zilivyotumika,endeleeni kuwachukulia hatua
wanaoharibu kwa makusudi miundombinu ya maji na vyanzo vya maji’’,alisema
Mndeme.
Kwa
upande wake Meneja wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira vijijini (RUWASA)
Mkoa wa Ruvuma Mhandisi Rebman Ganshonga ameyataja majukumu ya RUWASA kuwa ni kuandaa
mipango ya kusanifu miradi,kujenga na kusimamia uendeshaji wake.
Majukumu
mengine ni kuendeleza vyanzo vya maji kwa kufanya utafiti wa maji chini ya
ardhi,kuchimba visima na kujenga mabwawa sanjari na kufanya matengenezo makubwa
ya miundombinu ya maji.
MWISHO
Comments
Post a Comment