Na. Revocatus Kassimba, KAHAMA
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ameipongeza Wizara
ya Kilimo kwa kuweka mkakati wa kuhakikisha nchi inajitosheleza kwa ngano huku
akiagiza mashamba yote yaliyokuwa ya serikali na sasa hayatumiki kuzalisha
ngano yawekewe utaratibu wa kugawiwa kwa wakulima.
Rais
Magufuli ametoa maagizo hayo leo (28.01.2021) Chapulwa mjini Kahama wakati
alipoweka jiwe la msingi la ujenzi wa kiwanda cha vinywaji baridi na
vifungashio vinavyomilikiwa na kampuni ya KOM Group ya wazawa chini ya
Mtanzania Mhoja Nkwabi.
”
Nimefurahi kuona Wizara ya Kilimo imeanza kuweka mkazo kwenye uzalishaji wa
ngano ili suala la kuagiza zaidi ya tani milioni moja nje ya nchi na kufanya
nchi itumie fedha nyingi za kigeni liishe” alisema Rais Dkt. Magufuli.
Aidha
,Rais Dkt. Magufuli ameagiza mashamba yote yaliyokuwa ya serikali
yaliyokusudiwa kwa kuzalisha ngano na sasa hayalimwi, wizara ya kilimo
ihakikishe wamiliki wake wanayalima vinginevyo yagawiwe kwa wawekezaji wenye uwezo na
wakulima wadogo.
“Yale
mashamba yasiyotumika kuzalisha ngano na ni ya serikali tuyalime yote, wawekezaji
wapewe kulima ngano hata ikibidi tuyatoe bure” aliagiza Rais Dkt. Magufuli.
Awali
akizungumza kwenye halfa hiyo Waziri wa Kilimo Prof. Adolf Mkenda alimpongeza
Rais Magufuli kwa uthubutu wake na
maelekezo yake kuhusu nchi kujitosheleza kwa zao la ngano na kuahidi wizara itaendelea
kutekeleza maagizo ya Rais.
Prof
Mkenda alieleza kuwa kwa sasa nchi inazalisha wastani wa tani 60,000 za ngano
huku ikiingiza toka nje tani takribani milioni moja kwa mwaka wakati Tanzania ina ardhi nzuri inayofaa kwa
uzalishaji zao hilo ndio maana Wizara yake imeweka mkakati maalum wa kuhakikisha
baada ya miaka miwili nchi inajitosheleza kwa ngano hapa .
“Tumekubaliana
na wawekezaji na wafanyabiashara wakubwa wa ngano kwa hiari kuwa kuanzia mwaka
huu wataanza kununua ngano ya wakulima wa ndani kwa bei ya Shilingi 800 kwa
kilo na kama wataagiza nje kiwango cha asilimia 60 basi watapaswa kununua
kiwango kama hicho hapa nchini ili kutoa fursa kwa wakulima kupata soko “
alisisitiza Prof. Mkenda.
Katika
hatua nyingine Prof. Mkenda amemweleza Rais Magufuli kuwa Wizara ya Kilimo
itashirikiana na Wizara ya Viwanda na Biashara kutafuta soko la uhakika la
mchele wa wakulima wa Kahama ambao ni wazalishaji wakubwa .
Prof.
Mkenda aliongeza kusema Wizara ya Kilimo inauona mji wa Kahama kuwa ni kituo
maalum cha kiuchumi kwa kuwa ipo karibu na mipaka ambayo ikitumika vizuri
itasaidia kutoa fursa ya masoko ya mazao ya kilimo .
Waziri
huyo wa Kilimo amewapongeza kampuni ya KOM Group kwa uwekezaji utakaotoa fursa
ya mazao ya kilimo ikiwemo maembe, machungwa, mapera na mazao ya mpunga na mahindi kuongezwa
thamani pia ajira zaidi ya 400 za kudumu na 1000 za muda.
“Baadhi
ya mpunga wetu unavuka mipaka na kwenda kuchakatwa huko badala ya hapa Kahama, hivyo
tunahitaji kuona wawekezaji wengi kama KOM Group wakianzisha viwanda vya
kuchakata mazao ya kilimo na kuyasindika hapa nchini ili wakulima wanufaike na
kuwa uhakika wa kipato” alisema Prof. Mkenda.
Naye
Waziri wa Viwanda na Biashara Cecil Mwambe amekishauri kiwanda cha KOM Group
cha Kahama kutumia fursa ya uwepo wa korosho ghafi nyingi nchini kuanza
kuchakata bidhaa zitokanazo na korosho kwani zina soko kubwa ndani na nje.
“Wananchi
wa Kahama tumieni fursa ya kiwanda hiki
cha KOM Group kuuza malighafi ili kuongeza kipato na uwezo wa kiwanda kuzalisha
bidhaa hali itakayokuza uchumi wa nchi “ alisema Mwambe
Rais
Dkt. John Pombe Magufuli yuko ziarani Mkoa wa Shinyanga kukagua shughuli za
maendeleo pamoja na kuongea na wananchi.
Mwisho.
Imeandaliwa
na ;
Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Wizara ya Kilimo
KAHAMA
28.01.2021
Comments
Post a Comment