Na. Albano Midelo, Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma
MKOA
wa Ruvuma umelenga kupanda miti ya biashara katika eneo lenye ukubwa wa hekta
40,000 hadi kufikia mwaka 2025.
Mshauri
wa Maliasili na Utalii wa Mkoa wa Ruvuma Afrikanus Challe amesema mradi huo unatekelezwa kwa miaka kumi kuanzia
mwaka 2015,unatekelezwa kwa kupanda miti maeneo ya serikali kuu,serikali za
mitaa,vyuo,shule na vijiji.
Challe
ameitaja aina ya miti inayopandwa ni ile ambayo inafaa kwa ajili ya malighafi
za viwanda vya mazao ya misitu ambayo ni misindano (pine) milingoti (Eucalyptus)
na misaji (Teak).
‘Hadi
kufikia mwaka 2020 jumla ya miti ya biashara iliyopandwa na wakala wa Huduma za
misitu Tanzania (TFS) ni msitu wa hekta 4785, Halmashauri zilipanda miti hekta
425, vyuo na shule hekta 420 na watu binafsi hekta 23,964.
Amesema
jumla ya mashamba yote ya miti yaliyopandwa katika kipindi hicho ni hekta
29,194 sawa na asilimia 56.1 ya lengo.
Kwa
mujibu wa Mshauri huyo wa Maliasili na Utalii,Mkoa wa Ruvuma unalenga kuanzisha
mashamba mapya mawili ya miti ya misaji katika Wilaya za Tunduru na Nyasa.
Kwa
upande wake Mratibu wa kuendeleza Program ya mnyororo wa thamani wa mazao ya
misitu(FORVAC) Mkoa wa Ruvuma Marcel Mtunda
amesema wameandaa miche ya miti
ya biashara aina ya misaji,pine na Eucalyptus ipatayo 4,000,000 ambayo
itapandwa maeneo maalum yaliyotengwa na Mkoa yakiwemo Ifinga, Liuli, Liumbe,
Upolo, Mpepo, kipiki na Kihangamahuka.
Amesema
Mkoa unatekeleza mradi wa kuongeza thamani mazao ya misitu na nyuki kwa
kushirikiana na FORVAC na kwamba mradi unatekelezwa katika wilaya zote tano za
Mkoa wa Ruvuma.
“Mradi
huu utawezesha vijiji kutunza misitu ya hifadhi ya vijiji na kuwawezesha kupata
faida kwenye misitu hiyo,hadi sasa wilaya ya Tunduru imeshapata mashine moja ya
kuchana mbao ambayo imeanza kufanyakazi katika kijiji cha Sautimoja’’, alisema
Mtunda.
Hata
hivyo amesema Mkoa kwa kushirikiana na FORVAC imeomba mashine nyingine tatu ili
zitumike katika wilaya za Namtumbo,Songea,Mbinga na Nyasa na kwamba mradi
utasaidia kupunguza gharama za serikali kutekeleza miradi ya kimkakati ya
kujenga shule,zahanati na madawati.
Comments
Post a Comment