FAHAMU HISTORIA YA ZAO LA ZABIBU DODOMA NA MAAJABU YAKE

 


Na Pendo Mangala, Dodoma

Mkoa wa Dodoma ni miongoni mwa  Mikoa  ya Tanzania  wenye postikodi namba 41000,uko katikati ya nchi na umepakana na Mikoa ya Manyara,Morogoro,Iringa na Singida ambao pia ndio Makao makuu ya Nchi na Serikali.

Eneo lote la Mkoa lina jumla ya kilomita  41,310. Sehemu kubwa ni nyanda za juu  kati ya mita  830 hadi 2000.

Kilimo cha Zabibu Mkoani Dodoma kina historia ndefu, ambapo kwenye miaka ya 1950 na mwaka 1974 chini ya uzaidizi wa bihwana misheni, serikali ya Tanzania wakati huo ikishirikiana na serikali ya china ilianzisha kituo cha kilimo cha Bihawana Farmers Training Center (BFTC) kwa ajili ya kufundisha Wakulima juu ya kilimo cha Zabibu na mazao mengine.

Dodoma ndio mkoa pekee unaolima Zabibu kwa wingi nchini Tanzania na hata kwa Afrika mashariki ndio mkoa wenye utajiri mkubwa wa zao hili.


Licha ya zao la Zabibu kulimwa katika maeneo mbalimbali nchini kama zao la biashara na kuwa sehemu ya kujipatia kipato na kukuza Uchumi wa Taifa kwa ujumla kwa wakulima wengi lakini kwa Mkoa wa Dodoma limeonekana kutia fola.

 Hiyo ni kutokana na Dodoma  kubainika kuwa sehemu ya kipekee Nchini yenye sifa ya kuzalisha zabibu zenye kiwango Cha ubora.

 

Stellah Hangambagi ni Mtafiti  wa kilimo kutoka Kituo Cha utafiti wa Kilimo TARI-Makutupora  anasema  kuwa hali ya hewa ya Dodoma ni nzuri na hivyo Zabibu hustawi zaidi.

 

Anasema  sifa ya kwanza ambayo imepelekeza Zabibu kustawi na kumea vizuri ni kutokana na Hali ya hewa ya Dodoma ambayo inapata mvua kiasi na jua kali jambo ambalo linaipa uwezo zabibu hiyo kuzaa Sana.

 

Anaitaja sifa nyingine   iliyopo Mkoani humo Zabibu inayolimwa huvunwa mara mbili kwa Mwaka Februari na Agosti tofauti na Mikoa mingine ambayo huivuna Mara moja tu.

 

"Zabibu ni fahari ya Dodoma kwasababu Zabibu hiyo ina uwezo wa kuzaa Mara mbili kwa Mwaka na ina ubora na mkulima anapata faida kubwa”,änasema.

 

Mtafiti huyo anafafanua kuwa wamekuwa wakiongeza thamani ya mazao katika  zabibu kama kutengeneza mvinyo,kutengeneza viungo pamoja na keki.

 

“Kilimo cha zabibu kinahitaji mvua za wastani japokuwa Dodoma inajulikana kwa ukame ila ardhi yake ina hifadhi maji kwa kipindi kirefu sana kwahiyo kwa mvua zinazonyesha kuanzia Disemba mpaka machi zinatosha kwa kuhudumia mizabibu mpaka mwezi wa julai kulekea kipindi cha mavuno,”anasema.

Kuna aina tatu za Zabibu ambazo ni Zabibu za mvinyo,Zabibu za mezani na Zabibu za kukausha ambazo zote zinazalishwa Dodoma ambapo anasema  Zabibu zinazozalishwa sana Dodoma ni za mvinyo zikifuatiwa na za mezani.

 

Sambamba na hilo anasema wamekuwa wakitoa mafunzo  kwa wakulima na wadau mbalimbali namna ya kutumia Teknolojia kwa kuwaalika kuwapa mafunzo namna yakutumia teknoljia kuanzia kuandaa shamba hadi kulima ili kuwa na kilimo chenye tija.

 

Anasema katika kipindi cha mwaka 2020wametoa mafunzo juu ya zao hilo kwa wakulima wapatao 3500.

 

Mtafiti huyo anasema  katika maonesho ya nanenane wamekuwa wakitoa elimu kwa wakulima mmoja mmoja na wadau kwa ujumla namna ya kutumia teknolojia katika zao la zabibu.

 

“Kitaifa Tari makutupora tumepewa jukumu la zao la zabibu lakini tunazalisha mazao mbalimbali ikiwemo Mihogo Karanga na korosho hivyo tunatoa wito watu kuja kujifunza na kununua pia,”

 

Wanashamba eneo la nanaenae kumekuwa na Watafiti wakitoa mafunzo muda wote na hata wakati wa  maonyesho ya nane huku akiishukuru COSTECH kwakuwaunganisha na waandishi wa Habari kwani wataweza kulitangaza zao hilo .

 

Sada Hussein ni Mratibu wa utafiti na ubunifu anasema kituo hicho cha TARI Makutupora tayari kimetoa kiasi Cha udongo,Mbegu za mvinyo na Teknolojia za usindikaji ikiwemo kukausha pamoja na dawa za  kunyunyuzia kwenye Mimea ya zabibu. 

 

Anasema gharama  za uzalishaji Zabibu zinatokana na suala zima la Uendeshaji wa shamba ambapo Kuna umwagiliaji na kutegemea mvua na wakati mkulima anaanza atapata hasara .

 

 Pia  Mkulima ambaye anatumia mvua atawekeza milioni 10.6kwaajili ya kulima zao hilo huku  kwa  mkulima anaye tumia umwagiliaji   atatumia Shilingi milioni3.

 

Mratibu huyo anafafanua kuwa   mkulima huyu ambaye anatumia mvua atavuna  kilo3500 kwa hekari moja kwa Mwaka na anae mwagilia atavuna  kilo 8500 kwa hekari moja.

 

Naye Devotha mchau toka Idara ya uchumi kilimo  anaehusika na Sayansi ya Jamii ambaye pia anashughulikia masoko na uwekezaji kwa mkulima katika zao la Zabibu anasema kwa Mkulima  anaetegemea mvua  tathmini ya haraka atavuna wastani wa tani 4  lakini anaetumia umwagiliaji  anavuna  tani10 na kuwashauri wakulima kutumia teknojia ya  umwagiliaji na kutumia teknolojia ya kisasa.

 

Anaeleza bei ya soko hasa kwa Mbegu ya waine ni shilingi  1000 kwa kilo  hadi 1500 lakini Zabibu za matunda kabla ya kuchakatwa ni sh3000 hadi 3500.

 

Hata hivyo amesema Serikali imekuwa ikifanya tihada mbalimbali  katika kuwawezesha wakulima wadogo kwa kuanzisha mashamba darasa Kata ya Gawaye,Chinangali na Chamwino lakini kwa Dodoma mwitikio bado mdogo kutokana na changamoto ya utunzaji Zabibu kuwa na gharama  kubwa.  

 

Anasema kutokana na Utafiti uliofanyika mkulima anaweza kupata ongezeko la  faida hadi asilimia 50 endapo atatumia teknolojia ya kisasa.

Naye Mkurugenzi wa Taasisi ya utafiti wa kilimo TARI Makutupora,Dk.Cornel Massawe anasema wapo katika hatua za mwisho kukamilisha utafiti wa aina tano za mbegu za Zabibu zitakazosaidia  kuongeza uzalishaji.

Massawe anasema  wanaamini Mbegu hizo zitakuwa bora zenye vigezo na zinazotakiwa kwa mkulima ili kuongeza tija katika sekta ya kiimo ambazo zitakuwa na uwezo wakuzalisha tani 24 kwa hekta moja.

 

Anazita aina hizo za Mbegu kuwa ni Gegina,beauty,Seedless,Ruby seedless,Alphonce Lavee na  Strah ambazo zinahimili mabadiliko ya tabia nchi kama vile ukame,mafuriko pamoja na ukame.

 

Aidha amebainisha kuwa ili kuleta tija  katika kilimo hicho cha Zabibu,Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Sayansi na teknolojia COSTECH wamepokea kiasi cha Shilingi Milioni297zitakazo tumika kuboresha kiwanda kidogo cha kuchakata zabibu.

 Pia wamekuwa wakitoa mafunzo ya ziada ya kuchakata juisi inayotokana na zabibu ili kuzuia upotevu wa zao hilo baada ya kuvuna.

“Tumewapa wakulima elimu ya kuchakata Zabibu  lengo ni kuhakikisha wanapata tija katika kuinua vipatao vyao,”amesema.

Mkurugenzi huyo anaseleza kuwa baada ya wakulima kuchakata  Zabibu zao  wamekuwa wanauza kwenye kiwanda ambapo asilimia 80 ya watengenezaji wa juisi wamepata mafunzo toka TARI Makutupora.

Mwisho.

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.