VIJANA WA CHANG’OMBE,KIZOTA,MAILIMBILI,KIKUYU WAONYWA

 


Na Jackline Kuwanda, Dodoma.

Kuelekea katika msimu wa sikuku za mwaka mpya ,Jeshi la Polisi Mkoani Dodoma limepiga marufuku uchomaji wa matairi barabarani .

Wito huo umetolewa leo Mkoani hapa na Kamanda wa Jeshi hilo Gilles Muroto wakati akizungumza na waandishi wa Habari ambapo amesema kuwa vijana waliopo mitaa ya Chang’ombe,kizota,mailimbili na kikuyu wanapaswa kuachana na mchezo huo huku akiwataka wenyeviti wa mitaa katika maeneo yao kuhakikisha kwamba hakuna uvunjifu wa amani unaofanyika .

‘’vijana hao wanaokusudia kuchoma matairi tumesema ni marufuku kuchoma tairi barabarani kwanza wanaharibu miundombinu ya serikali kwahiyo kama unachoma miundombinu unatualika polisi tukushughulike kwahiyo tunawaagiza vijana hao kuachana na mchezo huo’’ Amesema Muroto  

Aidha, Kamanda Muroto amewataka madereva kuzingatia sheria za usalama barabarani huku akibainisha kuwa zipo operesheni zinazoendelea kwaajiliya kuwakamata wale wote watakao vunja sheria.

‘’akiona anakwenda kupata kinywaji au kwenye ulevi aache gari lake nyumbani ,akiondoka kwenda na gari kwenye ulevi ahakikishe anakunywa kwa kiwango kinachotakiwa akizidisha kiwango akapata ajali anaanza mwaka mbaya 2021 kwahiyo wao wachukue tahadhari ,bodabaoda pia operesheni zinaendelea wanaopakia mishikaki ,magari,ukimbiaji wa mwendo kasi , kusimama kwenye zebra ,magari ya  serikali yanayokimbia kwa kasi yote hayo tunazingatia kuhakikisha kwamba yanafuata sheria’’ Amesema Muroto

Hatahivyo ,Kamanda Muroto amesema Jeshi hilo kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama wamejipanga kuimarisha ulinzi katika msimu huu wa sikuku za Mwaka mpya kwenye maeneo mbalimbali ikiwemo Nyumba za Ibada ,Barabarani na kuendelea.

Mwisho.

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.