Na. Mwandishi Wetu, DODOMA
Waziri wa Kilimo, Prof. Adolf Mkenda amesema kipaumbele chake ni kuona wakulima wanaongeza tija kwenye uzalishaji wa mazo nchini kwa kutumia eneo dogo kuzalisha mazo mengi zaidi na kukuza uchumi wa kaya na taifa.
Waziri wa
Kilimo amesema hayo wakati akikakabidhiwa rasmi ofisi na aliyekuwa Waziri wa
Kilimo, Japhet Hasunga hafla iliyofanyika makao makuu ya wizara ya Kilimo
Mtumba jijini Dodoma.
Hafla ya
makabidhiano imefanyika kufuatia uteuzi uliofanywa na Rais Dkt. John Pombe
Magufuli kumteua Prof. Mkenda kuwa Waziri wa Kilimo katika awamu hii ya pili ya
uongozi wa serikali ya awamu ya tano.
“ Sekta ya
kilimo inachangia asilimia 28 ya pato la taifa lakini sekta ndogo ya mazao
inachangia asilimia 18 ambapo tija ni ndogo. Tija kwenye kilimo ni ndogo sana
wakati theluthi mbili ya watanzania inategemea kilimo kwenye maisha ambapo
asilimia karibu 70 imejiali huko” alisema Prof. Mkenda.
Katika salamu
zake Mhe. Hasunga amesema anamshukuru Rais Magufuli kwa kumwamini na kumteua
kuongoza wizara ya kilimo kwa miaka miwili ya awamu yake ya kwanza na kuwa
alifanya kazi kuhakikisha nchi inakuwa
na utoshelevu wa chakula.
“Nimefanya kazi
miaka miwili kama Waziri wa Kilimo, nafurahi katika kipindi chote cha kwanza cha awamu ya
tano nchi imeweza kujitoshelevu kwa
chakula” alisema Hasunga.
Hasunga alisema
mafanikio hayo yamechangiwa kwa kiwango kikubwa na msukumo wa uongozi wa Rais
Magufuli pamoja na wakulima wa Tanzania waliotikia kauli mbiu ya kufanya kazi
kwa bidii.
Waziri huyo
mstaafu na mbunge wa Jimbo la Vwawa mkoa wa Songwe aliongeza kusema ataendelea
kuwa mwaminifu na kuiomba wizara ya kilimo kutilia mkazo suala la upatikanaji
wa pembejeo za kilimo ikiwemo mbegu bora, viuatilifu, mbolea na zana bora ili
kilimo kikue na kuchangia zaidi kwenye pato la taifa.
Kwa upande wake
Waziri wa Kilimo Prof. Adolf Mkenda alisema atahakikisha sekta ya kilimo
inaongeza kuchangia ukuaji wa uchumi toka wa sasa wa asilimia 28 hadi zaidi
huku sekta ya kilimo mazao ikitoa mchango mkubwa kwenye upatikanaji wa
maligahfi za viwanda.
Katika kuhakikisha
sekta ya kilimo inatoa mchango mkubwa kwenye kwenye ukuaji wa uchumi nchi, Prof
.Mkenda maetaja mambo makuu manne ambayo ni diara kwake wakati akiongoza Wizara
ya Kilimo.
Kwanza kuongeza
tija kwenye uzalishaji wa mazao ya kilimo kwa kutumia eneo dogo kuvuna mazao
mengi hivyo taasisi ya utafiti (TARI) na wakala wa mbegu (ASA) wana jukumu la
kuongoza kwenye utafiti wa mbegu bora nyingi ili wakulima wazalisha zaidi.
Pili, kusimamia
na kuelimisha mbinu bora za uzalishaji (Good agricultural practices) ambapo
amelenga kufanya umwagiliaji kwa njia ya matone ukue na kuchangia kwenye
uhakika wa chakula ikiwemo upatikanaji wa viutalifu na huduma za ugani kwa
karibu zaidi.
Mkakati wa tatu
Prof. Mkenda ameutaja kuwa ni upatikanji wa masoko ya uhakika wa mazao ya
wakulima kwa kusimamia masoko ya kimkakati na kufanya wakulima wanufaike na
jasho lao kwa faida huku nchi ikiwa na uhakika wa chakula na malighafi.
Mwisho Prof
Mkenda amesema katika uongozi wake ndani ya wizara ya Kilimo atahakikisha
upatikanaji wa mitaji na uwekezaji kwenye kilimo unaluwa rahisi na wenye
kunufaisha makundi ya vijana na wawekezaji ambapo atatoa mkazo kwenye
upatikanaji wa mitaji kupitia miko yenye riba nafuu toka taasisi za fedha
nchini na zile za nje ya nchi.
Ka upande wake
Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Gerald Kusaya alisema kuwa wizara hiyo inazo
changamoto ikiwemo kuhakikisha nchi inajitosheleza kwa upatikanji wa sukari
ambapo wa sasa upungufu ni zaidi ya tani 60,000 kila mwaka na upande wa
upatikanaji mafuta ya kula upungufu ni zaidi la tani 365,000.
Kusaya alitoa
wito kwa viongozi wakuu wa wizara wapya kushirikiana na watumishi ili
kuhakikisha lengo la serikali ya awamu ya tano la kufikia hekta milioni moja na
laki mbili zinafikiwa na kufanya sekta hiyo ichangie zaidi kwenye ukuaji wa
uchumi kwani Tanzania ina eneo la hekta milioni 29 zinazofaa kilimo cha
umwagiliaji kati ya hekta milioni 44 zinazofaa kwa kilimo.
Mwisho.
Comments
Post a Comment