Na. Abdul Rahman Salim,
Wakati Utekelezaji wa lengo la
Serikali kupitia Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) la kuweka mfumo
wa kisasa wa kutunza mazao kufikia asilimia 80. Wakala hao wameshauriwa
kujiandaa kununua mahindi mengi Zaidi ili kuwahakikishia wakulima soko la mazao
yao katika kipindi cha msimu wa 2020/2021.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim
Wangabo amesema kuwa ni vyema NFRA wakaongeza fedha za kununua mahindi na kisha
kutafuta soko nje ya nchi hasa katika nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa
Afrika (SADC) Pamoja na nchi nyingine ili kuwapa fursa wakulima nchini kufanya
biashara na NFRA ili kuepuka kuhangaika kutafuta soko la mazao yao.
“Mkoa wa Rukwa tumezalisha tani za
mahindi tani 585,000 na matumizi yetu ya ndani ni tani 291,000 kwahiyo tulikuwa
tuna ziada ya tani 294,000, sasa ukiangalia kwamba tani 294,000 halafu mahindi
yananunuliwa tani 11,000 kwahiyo mahindi mengi yalibaki ndio kikawa kilio cha
wakulima wa mkoa wetu wa Rukwa kwahiyo nategemea kwamba ukamilishwaji wa
vihenge hivi NFRA itakuwa na uwezo wa kuchukua tani 58,500, hii kwa sisi mkoa
wa Rukwa ni sawa na kuingiza na kutoa ili wawauzie watu wengine.”
“Kwahiyo niwaombe NFRA ndio wamekuwa
mkombozi sasa kwa wakulima, mjipange vizuri ili kuongeza fedha muweze kununua
mahindi mengi kwa wakulima vinginevyo wakulima watakata tamaa na sasa
wanaendelea kuzalisha baada ya kuona kwamba hivi vihenge hapa vinakwenda
kukamilika kwahiyo uwezo wa NFRA utakuwa mkubwa Zaidi wa kununua mahindi kwa
wakulima, ninyi mnao uwezo wa kuona wapi muyapeleke hayo mahindi, ninyi mfanye
biashara na nje na sisi tufanye biashara na nyie,” Alisema.
Kwa upande wake Mhandisi Mkazi kutoka
Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Mhandisi Haruna Kalunga amesema kuwa hadi
tarehe 28.12.2020mkandarasi ameshatumia muda wake wa miezi 15 sawa na asilimia
83 ya muda aliopewa kwenye mkataba huku utekelezaji ukiwa ni asilimia 80 na
hivyo kuufanya mradi kuwa nyuma kwa asilimia 3 na kuongeza kuwa ucheleweshwaji
huo umechangiwa na kucheleweshwa kwa msamaha wa kodi wa vifaa vinavyotoka nje
ya Tanzania.
Kwa mkoa wa Rukwa mradi huo
unatekelezwa na Mkandarasi Unia Araj kutoka Poland ikisaidiana na Mkandarasi
Mzawa Elerai kutokea Arusha kwa thamani ya Dola za marekani 6,019,399.00 ambayo
ni asilimia 30 ya mradi mzima unaotekelezwa katika mikoa mitatu Pamoja na Mkoa
wa Katavi na Manyara wenye jumla ya thamani yad ola za marekani 20,280,906.00.
Comments
Post a Comment