Wananchi wa Kata ya Naliendele walia na ukosefu wa maeneo ya kujengea huduma za kijamii.

 


Na Faruku Ngonyani,Mtwara

Wananchi wa kata ya Naliendele iliyopo Halmashauri ya Manispaa Mtwara Mikindani Mkoani Mtwara wamelalamikia juu ya ukosefu wa maeneo ya kujenga maeneo ya huduma muhimu za kijamii kama vile Shule, eneo la makaburi ,Soko pamoja eneo la zahanati.

Hayo wameyazungumza mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Dunstani Kyobya kwenye Mkutano wa hadhara uliyofanyika katik eneo hilo ukiwa na lengo kwa Mkuu wa Wilaya la kusikiliza na kutatu kero za wananchi hao.

Wananchi hao wamesema kuwa kwa sasa wanakosa maeneo ya huduma ya kijamii kwa kuwa maeneo yaliyo mengi yamechukiliwa na Taasisi mbalimbali za kiserikali wakiwemo baadhi yao kiwa ni kituo cha Utafiti cha Kilimo Naliendele,Chuo cha Kilimo,jeshi la wananchi pamoja na mamlaka ya uwanja wa Ndege.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Dunstani Kyobya ametoa mwezi mmoja kwa wataalam wa ardhi kutoka Halmashauri ya Manispaa Mtwara Mikindani kuhakikisha wanaenda kufanya utafiti ili maeneo hayo yaweze kupatikana na wananchi waweze kujenga nyumba za  kupata huduma muhimu za kijamii na makazi yao.

Aidha Mkuu huyo wa Wilaya ametoa agizo kwa Chuo cha utafiti cha kilimo Naliendele kutoa elimu kwa wananchi wa kata hiyo ya Nalinendele ili waweze kufahamu na kujua umuhimu wa kuwa na chuo hiko katiuka eneo hilo.

Lakini pia Mkuu huyo wa Wilaya ametoa wito  kwa Mkurugenzi wa   Manispaa Mtwara Mkindani kutoa Notes ya miezi kwa Mtu yeyote asiyeendeleza maeneo yao na hatmae kunyang’anywa maeneo yao.

“Wale wote ambao wanamaeneo yao hayajaendelezwa  wenye hati na wasikuwa na hati kanini wasipewe notes ya kunyang’anywa maeneo hayo kwa kutoyaendeleza’’

MWISHO.

 

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.