WALIMU WAPYA WATAKIWA KURIPOTI NDANI YA SIKU 14

 




DODOMA.

SERIKALI imeajiri walimu wapya wa shule za msingi,sekondari  pamoja na mafundi  sanifu wa maabara elfu 13 huku ikiwataka walimu hao kuripoti katika vituo vyao vya kazi walivyopangiwa ndani ya siku 14 kuanzia disemba mosi mwaka huu.

Miongoni mwa walioajiriwa asilimia 60 ni walimu wa shule za msingi wakiwemo walimu wenye shahada 1,100 na asilimia 40 ni walimu wa shule za sekondari.

Akizungumza na Waandishi wa Habari jana Ofisini kwake jijini Dodoma Katibu Mkuu,Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali (TAMISEMI) Mhandisi Joseph Nyamhanga amesema ajira hizo zinatokana na kibali kilichotolewa na Rais Dokta John Magufuli septemba 7 mwaka huu.

Mhandisi Nyamhanga ametoa maelekezo matano kwa waajiriwa hao wapya ikiwemo kuhakikisha wanaripoti katika eneo walilopangiwa kwak uwa hakuna mwajiriwa atakayebadilishiwa kituo kwa kipindi cha miaka mitatu.

Waajiriwa hao wanatakiwa kuripoti wakiwa na vyeti halisi vya taaluma vya kidato cha nne na kidato cha sita, vyeti halisi vya kitaaluma vya kuhitimu mafunzo ya ualimu ya ngazi husika,kitambulisho cha Taifa au namba ya utambulisho ya NIDA na cheti halisi cha kuzaliwa.

Mwisho.


Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.