TAHADHARI KUHUSU WAGONJWA NA NDUGU ZAO WANAOCHANGISHA FEDHA ZA MATIBABU YA MOYO KWA AJILI YA KUTIBIWA KATIKA TAASISI YA MOYO JAKAYA KIKWETE (JKCI)

Uongozi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) unapenda kuutahadharisha Umma kuwa waangalifu na wagonjwa wanaochangisha fedha kwa ajili ya kutibiwa katika Taasisi hii.


Ndugu Mwananchi, inawezekana wagonjwa hao wanaochangisha fedha za matibabu wanakuwa tayari wamepata msamaha wa matibabu kutoka kwa Taasisi au wasamaria wema wamewalipia.

 

Hivi karibuni kumezuka tabia ya baadhi ya wagonjwa au ndugu zao ambao siyo waaminifu wanachangisha fedha za matibabu kwa wananchi wakati tayari wameshapata msamaha wa matibabu kutoka kwa Taasisi au kutokuwa na tatizo ambalo gharama za matibabu yake zinahitaji kiasi kikubwa cha fedha.

 

Kama utakutana na tangazo la aina hiyo kabla hujamsaidia mhusika tafadhali wasiliana na uongozi wa Taasisi kupitia namba 0222152392/0782-042010/0688-027982 ili kupata ufafanuzi.

 

 

Imetolewa na:

 

 

 

Anna Nkinda

Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano

Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete

27/11/2020

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.