NDUGAI AMUONYA MBOWE

 


Na Jackline Kuwanda, Dodoma

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mh Job Ndugani amesema ni jambo lisilokubalika kwa mtu yeyote kudharau shughuli za Bunge ,kudhalilisha Bunge,kudhalilisha uongozi wa Bunge na hata kudhalilisha wabunge ambao tayari wamekwisha kuapishwa.

Ndugai ameyasema hayo leo Jijini Dodoma katika Hafla ya uapishaji wabunge wateule katika viwanja vya Bunge jijini hapa.

Aidha Ndugai amesema wabunge wote walioapishwa wanatambulika kama wabunge halali wa Bunge la 12 wakiwamo wabunge 19 wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA.

Wakati huo huo Mh Ndugai amewataka watanzania kupiga vita ukandamizaji dhidi wanawake katika jamii zao kwa kisingizio chochote kile huku akimuonya Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kwa kitendo cha kutoa maneno ambayo si mazuri dhidi ya wanawake walioapishwa hivi karibuni akiwemo Halima Mdee pamoja na wenzake.

''ni aibu kubwa kutukana wanawake hadharani napenda kumuonya na kumkanya mwenzangu asione sifa katika jambo hilo wanawake ni mama zatu,dada zetu,shangazi zetu hata kama wamekosea namna gani tuwatafute tukae nao,tupate  maelezo yao na sio kuwafukuza kama vibaka'' Ndugai  

Hatahivyo, Mh Ndugani ametoa wito kwa waandishi wa Habari  kuwa na weledi ya kutosha kuhusu  shughuli za Bunge  na  kutokuwa sehemu ya kisikiliza upotoshaji unandolea.

MWISHO.

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.