HPSS KUBORESHA MFUMO WA AFYA NCHINI

 

Na Rhoda Simba Dodoma.

MRADI wa Tuimarishe afya wa (HPSS) unaofadhiliwa na Serikali ya Uswis chini ya shirika la Maendeleo la SDC Swis Agency For Development and Copperation umejipanga kuboresha mfumo mzima wa afya nchini kwa kutekeleza miradi mbali mbali kupitia serikali.

Ally Abdallah


Hayo yamesemwa leo jijini Dodoma na Meneja mradi Ally Abdallah wakati akizungumza na waandishi wa habari katika kongamano la saba la wadau wa afya nchini (Tanzania Health Summit).

Aidha, amesema kuwa lengo la mradi huo ni kutekeleza miradi  ambayo italeta matokeo chanya na kuonekana katika jamii na unafanya  uboreshaji  katika mfumo wa afya, mfumo wa fedha, mfumo wa vifaa tiba, na mfumo wa upatikanaji wa dawa.

“Mfano wa mifumo hiyo ni pamoja na CHF iliyoboreshwa mfumo wa upatikanaji wa dawa (Jazia PVS)na Mradi huu upo hapa katika maonesho ili kuchangia tija katika masuala mazima ya mfumo  wa afya nchini, kuchangia mifumo ya afya nchini, pamoja na kujifunza.” amesema Abdallah.

“Kwa kuwa kila tunachokifanya lazima kilete matokeo kwahiyo sisi tupo hapa ili kuonesha  miradi tuliyoifanya na si vinginevyo” amesema Abdallah.

Amesema Mradi wa Tuimarishe Afya (HPSS,) ni mradi mkubwa na wenye mafanikio kwani upo hadi kwenye ilani inayozungumzia upatikanaji wa dawa nchini.

Hata hivyo Abdallah amesema wao wamejipanga kuendelea kutoa elimu  katika banda lao kwenye kongamano hilo  la saba la  wadau wa afya  kwani kupitia wadau hao ndipo wanapopata fursa zaidi ya kuutangaza mradi na kujitangaza kwa jamii kwa ujumla.

Aidha, amesema mfumo huo unamsaidia mgonjwa kuhudumiwa kwakutumia na madai ya mgonjwa huyo anayotakiwa  kulipwa yanatumiwa bima ya Afya.

Pia amesema mfumo umeunganishwa na  mashine za maabara na mashine ya mionzi ambayo inasaidia kuondoa na kupunguza kabisa ubadhilifu wa fedha kwani mfumo huo unatoa taarifa moja kwa moja karika hositali husika kwa kila hatua huduma aliopata mgonjwa.

Amesema kuwa mfumo huo ni mfumo wa kitanzania uliotengenezwa na watanzania  ambao umesaidia kurahisisha kazi katika sekta ya afya nchini.

Aliongeza kuwa mbali hayo aliongeza katika kukuza uchumi wa kati lengo ni kuleta afya bora ambapo ni muhimu kuboresha miundo mbinu jambo ambalo litasaidia kupunguza idadi ya vifo vya mama na mtoto kwani mfumo huo umeunganishwa na maabara kuangalia maendeleo yake.

Katika hatua nyingine alisema mfumo huo kazi zake ni kurahisisha huduma ya afya kuanzia mapokezi hadi huduma nzima ayakayo pata mgonjwa hospitalini.

Aidha, aliongeza kuwa wameweza kupata mafanikio makubwa katika utaratibu wa afya huku wakiongeza ufanisi kwenye utendaji kazi ambapo pia  kufanya kazi kwa njia ya mfumo wa kielektroniki inayowasaidia madaktari .

 

MWISHO 

 

 

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.