WAZAZI WANAAMINI KUMPIGA MTOTO NDIO KUMFUNDISHA ADABU JAMBO AMBALO SI SAHIHI-MDENDEMI

 


DODOMA.

Tafiti zinaonyesha kuwa robo tatu ya watoto walio na umri kati ya miaka 2 hadi 4 duniani kotesawa na watoto milioni 300 wanakumbana na ukatili unaodhaniwa ni kuwafunza nidhamu kutoka kwa wazazi au watu wanaowalea wakiwa nyumbani.

Ripoti hiyo ni kulingana na shirika la kimataifa la kuhudumia watoto UNICEF ilioyotolewa mwaka jana ambapo inaeleza kuwa zaidi ya watoto milioni 250 wanakumbana na adhabu ya kupigwa pamoja na mateso mengine wanayofanyiwa majumbani pamoja na maeneo mengine wanayokusanyika kujifunza ikiwemo mashuleni.

Taswira ya Habari imezungumza na baadhi ya wazazi  jijini Dodoma ili kufahamu ni kwa namna gani wanaweza kuwafunza nidhamu nzuri watoto wao bila kuwafanyia ukatili  ambapo wamesema kuwa wazazi wengi wanaamini kuwa kumchapa au kumpiga mtoto ndio kumfunza nidhamu jambo ambalo si sahihi kwani  mtoto anaweza akafundishwa adabu nzuri pasipo kupigwa bali kwa kumuwekea misingi mizuri ya kutambua jambo jema na baya.

Kwa upande wake Mkaguzi Msaidizi wa dawati la jinsia na watoto wa jeshi la polisi Mkoani Dodoma Thelesia Mdendemi amewataka wazazi kujenga mazoea ya kumzungumza na watoto wao  mara kwa mara kwa kuwa hiyo itasaidia kuwajengea nidhamu nzuri bila kuwapiga au kuwapa adhabu .

Amesema kuwa wazazi wengi wanaamini  kuwapa adhabu au kuwapiga watoto wao ndio kuwafundisha adabu nzuri jambo ambalo sio sahihi kutokana na hali hiyo  kumuathiri zaidi mtoto kifikra na kimwili.

Suala la ukatili wa dhidi ya watoto linatokea kila mahali kwa sura tofauti tofauti kulingana na mazingira anayoishi mtoto ambapo ripoti ya shirika la watoto Duniani  inathibitisha dhana hiyo na kueleza kuwa watoto wanakutana na ukatili katika hatua zote za ukuaji wao katika mazingira wanayoishi.

Mwisho.

 

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.