WAKULIMA KIJIJI CHA LEGANGA WAMUANGUKIA RAIS MAGUFULI



Kongwa, Dodoma.

WAKULIMA wa kijiji cha Leganga wilayani Kongwa wamemuomba Rais kuingilia kati mgogoro uliopo wa muda mrefu kati yao na jamii ya wafugaji wa kimasai ambao wanaodaiwa kukata miche ya mikorosho iliyooteshwa ikiwemo na kulisha mifugo kwenye mashamba yao.

Ombi hilo limetolewa na mkulima Mashaka Chiloa kwa niaba ya wakulima hao walipokuwa wakizungumza na waandishi wa habari.

Chiloa alisema kuwa wanalazimika kumuomba Rais ili aweze kuwatatulia suala hilo ambalo limechukua muda mrefu wanalofanyiwa na wafugaji hao,ambao bila kujali wamekuwa wakikata miche hiyo waliyootesha ya mikorosho na kulisha mifugo hiyo kwenye mashamba wanayotumia kulima.

Alisema kitendo wanachofanyiwa cha kukata mimea na kulisha mifugo hiyo kwenye mashamba ya wakulima hao, kinaweza kuhatarisha amani na utulifu uliopo hapa nchini na kusababisha mapigano na mauaji ya kutisha toka pande zote mbili.

“Hivyo tunamuomba Rais wetu kututatulia suala hili ambalo linaloonyesha kutoweka kwa amani na utulivu kutokana na vurugu tunazofanyiwa na wafugaji hao kwa kuwa hata usalama wa wakazi wa kijiji kuwa ni mdogo hivyo tunahitaji kuishi kwa usalama na sivyo vinginevyo” alisema.

Naye Jackson Makochi (80) mkulima wa kijiji hicho cha Leganga alisema kuwa serikali isipoingilia kitendo hicho cha wafugaji cha kuharibu mimea iliyooteshwa na wakulima,kinaweza kutokea mauaji ambayo yanayoweza kuhatarisha kukosa kuaminiana kati yao na sisi.

Makocho hata hivyo anasikitisha kuwepo kwa ukimia kuhusu suala hilo ambalo kwa viongozi wa ngazi ya wilaya tayari wameshatarifiwa kwa ajili ya kulitatua,lakini pia na wao wamekaa bila kulitolea uvumbuzi wowote.

“Wakulima wa kijiji hicho wanaweza kufikia mahali wakachoka kutokana na tabia hiyo wanayofanyiwa na jamii hiyo ya wamasai ya kukatiwa mimea yao mashambani pamoja na kulisha mifugo hiyo kwenye mashamba,sisi tunataka amani na utulivu na ndiyo maana tunamuomba rais wetu kutatua suala hili ambalo hivi sasa linazidi kuwa baya” alisema.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa serikali ya kijiji hicho cha Leganga Andason Chilingo akizungumza na waandishi habari kijijini hapo,alikiri kuwepo kwa mgogoro huo kwa muda mrefu kati ya pande zote mbili ya wakulima na wafugaji wa jamii ya kimasai wanaodaiwa kuharibu mimea mbalimbali na kuifyeka mikorosho huku mashamba yao wakichungia mifugo.

Alisema tatizo hilo lipo kwa wakazi wa kijiji hicho ambapo baadhi ya wafungaji wa kimasai wamekuwa na tabia ya kulisha mifugo yao kwenye mashamba ya wakulima na wakati huo huo wakifyeka miche ya mikorosho ambayo imepandwa kwa agizo la serikali katika wilaya hii ya Kongwa.

Chilingo alisema kuwa hivi karibuni mkulima mmoja wa kijiji hicho Mashaka Chiloa alifanyiwa vurugu kwenye shamba lake la hekari tatu la miche ya mikorosho kwa kuifyeka na huku mifugo yao wakilisha katika mashamba yao.

“Mimi kama mwenyekiti wa serikali ya kijiji ninakiri kuwepo kwa tukio hilo ambalo linalofanywa na wafugaji wa kimasai,ambao hivi karibuni wanifanikisha kukata miche ya mikorosho ya mkulima mmoja na kusababishia hasara kubwa ya mamilioni ya fedha, hivyo ninaiomba serikali yetu sikivu kuingilia kati suala hili ili kuepusha uvunjifu wa amani” alisema.

Mwenyekiti huyo wa serikali ya kijiji alisema kuwa kutokana na hovu iliyojengeka kati ya pande zote hizi mbili kuna hatari ya wakazi hao wakashindwa kulima mashamba yao kwa kuofia usalama wao,hivyo ninaiomba serikali kuchukua hatua za kisheria ili waweze kulimaliza tatizo hilo kwa amani na utulivu 

MWISHO

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.