VIONGOZI WA DINI WASHAURIWA KUWAHIMIZA WAUMINI KUWAOMBEA WANASIASA

 Na. Mwandishi Wetu, DODOMA

SHEKHE Bashart Rehman Butt wa Jumuiya ya kiislamu Tanzania amewaomba viongozi wa madhehebu ya dini kuwahimiza waumini wao kuwaombea wagombea wa vyama vya siasa watakaochaguliwa ili waweze kufanya kazi ya maendeleo kwa kushirikiana.



Aidha, maombi hayo pia yaambatane kwa wagombea hao kuwawezesha kuondoa utofauti zao za kiitikadi za vyama vyao vya siasa ili kusudi kila mmoja wake akawajibike kwa malengo ya kuliletea Taifa maendeleo.

Kiongozi huyo wa dini amesema hayo kwenye maadhimisho ya sherehe ya Maulid alipokuwa akizungumza na waandishi  wa habari mkoani hapa. 

Bashart alisema kuwa maombi hayo ni muhimu kwa viongozi hao watakaochaguliwa yatawawezesha pia kuondoa utofauti wao kawa kipindi walichokuwa kwenye mchakmchaka wa uchaguzi.

Hata hivyo Jumuiya hiyo ya Ahmadiyya imewaomba waumini wa dini ya kiislamu kusheherekea sikukuu hiyo ya Maulid kwa kuwakumbuka jamii ya watu wasiojiweza wenye mazingira magumu.

Alisema kuwa moja ya mafundisho ya Mtume Mohamadi ni pamoja na kuwakumbuka watu wasiojiweza,hivyo waumini wenye uwezo wanaombwa pia kuwakumbuka katika kipindi chote.

Mbali ya kusherehekea na jamii hiyo isiyojiweza pia waumini wanatakiwa kuwakumbuka wagonjwa mahosiptalini, wafungwa magerezani na watu wenye ulemavu ambao hawajiwezi kimaisha.

Aidha, amewataka waumini kutekeleza maadili ya kiongozi huyo kwa kuyafanya kwa vitendo ikiwa na kujiepusha na chuki na dharau kwa jamii inayowazunguka.

"Katika kipindi hiki cha sikukuu ya maulidi waumini siyo cha kuadhimishwa kwa kula vyakula na kunywa vivywaji,bali tunatakiwa kutekeleze maafundisho yake kwa ajili ya kujilinda na matendo maovu" alisema.

Alisema kuwa kuna makundi mengi hayana uwezo kwenye vipindi kama hivi vya sherehe,hivyo ni wajibu kwa waumini ambao wana uwezo kuwakumbuka ili na wao waweze kumkumbuka Mtume wao.

 

MWISHO

 

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.