Na. Mwandishi Wetu,
TUME ya haki
za binadamu na utawala bora (THBU) imeipongeza Serikali ya Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania kwa kulipa uzito tukio la uchaguzi mkuu kwa kukubali kutoa fedha za
kugharamia ili wananchi waweze kutimiziwa haki yao ya kikatiba.
Hayo
yamezungumzwa jijini hapa na Mwenyekiti wa Tume hiyo (THBU) Jaji Mstaafu Mathew Mwaimu wakati
akitoa tamko la tume hiyo kuelekea siku ya uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika
oktoba 28 mwaka huu.
Akitoa tamko
hilo,Mwenyekiti huyo amesema ,Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Uchaguzi na
Tume ya Uchaguzi Zanzibar imefanya maandalizi mazuri kwa mwendelezo wa
utoaji elimu ya uraia kwa wananchi kuhusu uchaguzi mkuu na kwa kusimamia vyema
hatua zote za mchakato wa uchaguzi kwa weledi huku zikizingatia sheria na
kanuni za nchi, haki, usawa, usalama na amani.
Kutokana na
hayo Jaji huyo mstaafu ametoa wito kwa wadau mbalimbali Wanapotekeleza majukumu
ya Uchaguzi mkuu wazingatie maadili, waheshimu haki za binadamu na misingi
ya utawala bora ikiwa ni pamoja na kuepuka matumizi makubwa ya nguvu yasiyokuwa
ya lazima.
“Tume
inawaasa wananchi wote raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuendelea
kutimiza wajibu wao wa kuzingatia sheria na kanuni za nchi kwa kuhifadhi amani
katika kipindi chote cha mchakato wa uchaguzi kwa maslahi ya
Taifa”anasema.
Akiongea kwa
niaba ya THBU, Mwaimu anasema Watanzania wote
waliotimiza vigezo kwa mujibu wa sheria, wanapaswa kutekeleza haki yao ya
kikatiba ya kupiga kura kuwachagua Rais, Wabunge, Wawakilishi na Madiwani.
“Hatua hii
muhimu imefikiwa baada ya kukamilika kwa mchakato wa miezi kadhaa uliohusisha
hatua za uhuishaji wa madaftari ya kudumu ya wapiga kura, uteuzi wa wagombea wa
nafasi mbalimbali na kampeni”anasema.
Licha ya
hayo,Mwaimu amesema tume hiyo inalipongeza Jeshi la Polisi kwa kulinda usalama
wa raia na mali zao katika kipindi chote cha mchakato wa uchaguzi.
Vilevile,
Tume inavipongeza vyombo vya habari kwa kuzingatia haki ya kikatiba ya wananchi
kwa kuwahabarisha kuhusu matukio na sera zilizokuwa zinanadiwa na wagombea na
vyama vyao na elimu iliyokuwa ikitolewa na wadau mbalimbali katika kipindi
chote cha mchakato wa uchaguzi.
“Jambo hilo
limetoa fursa kwa wananchi kuwasikiliza na kuwapima wagombea wa vyama
mbalimbali na litawasaidia kuchagua viongozi sahihi siku ya upigaji
kura”anafafanua Mwenyekiti huyo.
Hata hivyo
amelitaka Jeshi la polisi kuendelea kusimamia amani katika kipindi chote cha
uchaguzi ili watanzania waweze kutimiza haki yao ya kikatiba ya kupiga kura
katika hali ya utulivu na kuchagua viongozi bora.
“Sisi ka
Tume yenye dhamana ya kusimamia haki na utawala bora tunaliomba jeshi la polisi
linapotekeleza majukumu yake lizingatie maadili, kuheshimu haki za binadamu na
misingi ya utawala bora na kuepuka matumizi makubwa ya nguvu yasiyokuwa ya
lazima” anasisitiza.
Mbali na
hayo aliwasihi viongozi wa dini kuendelee kukemea maovu na kuliombea taifa
katika kipindi hiki muhimu ili haki, amani, utulivu na upendo viendelee
kudumishwa sasa na hata baada ya uchaguzi kumalizika.
Katika tamko
hilo ,Mwaimu pia amewataka Wagombea watakaoshindwa
katika kila
ushindani ni lazima awepo mshindi na atakaeshindwa, na kwamba wagombea
watakaoshindwa wanaombwa wakubali matokeo ili kudumisha amani ya nchi .
Mwisho
Comments
Post a Comment