JMP Ashinda Uchaguzi Mkuu 2020

Na. Mwandishi Wetu,  

MGOMBEA nafasi ya urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Dkt. John Magufuli ameibuka mshindi kwa zaidi ya asilimia 84 ya kura zote zilizopigwa.

Zoezi la Utangazaji wa Matokeo ya Jumla ya Uchagzui wa Rais 2020, likiendeleo katika Kituo cha Mikutano kimataifa Julisu Nyerere(JNICC), Jijini Dar es Salaam ambapo Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi (NEC), Mhe. Jaji Rufaa (Mst), Semistocles Kaijage


Kauli hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji Rufaa (Mst), Semistocles Kaijage alipokuwa akitangaza matokeo hayo katika kituo cha mikutano cha kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC), jijini Dar es Salaam.

Jaji Rufaa (Mst), Kaijage alimtangaza Dkt. John Magufuli wa CCM kuwa mshindi wa nafasi ya urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kupata kura zaidi 12,516,252 sawa na asilimia 84.4. “Kutokana na matokeo haya, namtangaza Dkt. Magufuli wa CCM, kuwa Rais mteule baada ya kuongoza kwa kupata kura nyingi kuliko wagombea wenzake” Jaji Rufaa (Mst), Kaijage.

Jaji Rufaa (Mst), Kaijage aliwataja wagombea wengine na kura zao kwenye mabano kuwa ni Queen Sendiga (ADC 7,627), Twalib Kadege (UPDP 6,194), Hashim Rungwe (CHAUMA 32,878), Mazrui Khalfan Mohamed (UMD 3,721), Seif Maalim Seif (AAFP 4,635) na Tundu Lissu (CHADEMA 1,933,271).

Wengine ni Mutamwega Mugahywa (SAU 14,922), Cecilia Mmanga (Demokrasia Makini 14,556), Maganja Jeremiah (NCCR Mageuzi 19,969), Prof. Ibrahim Lipumba (CUF 72,885), Philipo Fumbo (DP 8,283) na Bernard Membe (ACT-Wazalendo 81,129).

Akiongelea idadi ya waliojiandikisha kupiga kura, alisema kuwa ni 29,754,699, wakati idadi ya waliopiga kura ilikuwa 15,091,950 na kati ya hizo kura zilizokataliwa ni 261,755.

MWISHO

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.