JESHI LA POLISI KUENDELEA KUIMARISHA ULINZI NA USALAMA WAKATI WA MAJUMUISHO YA KURA




 DAR ES SALAAM.

Jeshi la Polisi kanda Maalum ya Dar es salaam limesema linaendelea kusimamia na kuimarisha ulinzi na usalama wakati majumuisho ya kura yakiendelea kutangazwa katika majimbo mbalimbali katika jiji hilo.

Kauli hiyo imetolewa jijini Dar es salaam na Kamanda wa Jeshi la Polisi kanda Maalum ya Dar es salaam Lazaro Mambosasa wakati akizungumza na waandishi wa akitembelea  vituo vya majumuisho ya kura Ili kuangalia hali ya ulinzi na usalama.

Kamanda Mambosasa amesema mji  wa Dar es salaam upo salama hivyo ni vyema wananchi wakaendelea kuwa watulivu na kusubiri kwani matokeo yanatoka baada ya kumalizika kuhesabiwa kwa kura.

Aidha Kamanda Mambosasa amesema wakati wa kampeni umepita hivyo atakaye karibu kuingia barabarani kwa lengo la kufanya vurugu watamchukulia hatua kali za kisheria.

 Baada ya watanzania hapo jana kushiriki katika Uchaguzi mkuu kupiga kura kuwachagua wabunge,madiwani pamoja na Rais sasa wametakiwa kuendelea kuwa watulivu wakati matokeo yakiendelea kutangazwa.

Mwisho.

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.