Dkt. Hussein Mwinyi: Rais mteule wa Zanzibar 2020-2025

Na. Mwandishi Wetu,

 

Tume ya uchaguzi Zanzibar imemtangaza Dkt. Hussein Mwinyi kuwa mshindi wa urais Zanzibar kwa kupata ushindi wa 76. 27% baada ya kumshinda mpinzani wake wa Chama cha ACT- Wazalendo Maalim Seif akiwa ni mshindi wa pili kwa kura 19.87%.

Dkt. Hussein Mwinyi
 

"Nimepokea ushindi kwa mikono miwili, nashukuru kuwa wananchi walio wengi wamenichagua mimi na chama changu cha Mapinduzi kwa miaka mitano ijayo,” alisema Rais mteule. Nawashukuru kwa uvumilivu na ustahamilivu mkubwa. Nawashukuru zaidi kwa kunipigia kura za kutosha kuwa rasi wa Zanzibar. Nitalipa imani hii kwa utumishi uliotukuka," alisema Dkt. Mwinyi.

Mwinyi ameeleza pia kuwa Zanzibar mpya itajengwa na Wazanzibari wote bila kujali itikadi, Zanzibar ni kubwa na muhimu kuliko tofuati hizo.

Rais huyo mteule aliwataka wafuasi wa chama chake kusherehekea kwa ustaarabu bila ya kukwaza wengine kwa kuwa ushindi wasingepata pasipo kuwa na ushindani.

 

MWISHO

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.