ANTHONY MAVUNDE AIBUKA KIDEDEA JIMBO LA DODOMA MJINI

 Na. Dennis Gondwe, DODOMA

Mgombea ubunge wa Jimbo la Dodoma mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Anthony Mavunde ameibuka mshindi katika Jimbo hilo lililopo ndani ya Jiji la Dodoma.

Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Dodoma Mjini, Wakili Msekeni Mkufya akitangaza matokeo ya Jimbo hilo


Akitangaza matokeo ya uchaguzi jimbo hilo, Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Dodoma mjini, Wakili Msekeni Mkufya amemtangaza Anthony Mavunde kuwa mshindi wa Jimbo la Dodoma Mjini.

Wakili Mkufya alisema kuwa Mavunde alipata kura 86,656 sawa na asilimia 86.44 akifuatiwa na Aisha Madoga wa CHADEMA mwenye kura 13,589 sawa na asilimia 13.50. 

Alisema kuwa jumla ya wananchi 335,324 walijiandikisha wakati waliopiga kura ni 102,769.

Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Dodoma Mjini, Wakili Msekeni Mkufya akimkabidhi cheti cha ushindi wa Jimbo hilo, Antony Mavunde wa Chama cha Mapinduzi kuwa mshindi wa Ubunge wa Jimbo hilo

MWISHO

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.