TRA DODOMA YAWAKUMBUSHA WAFANYABIASHARA KULIPA KODI YA MAPATO AWAMU YA TATU 2020.

 

Afisa Elimu na Huduma kwa Mlipa kodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania  TRA  Mkoa wa Dodoma Philipo Eliamini

Na Rahim Shaban, Dodoma.

Wafanyabiashara Mkoani Dodoma wametakiwa kuhakikisha wanalipa kodi ya awamu ya tatu kabla ya kumalizika septemba 30 mwaka huu ili kuepuka adhabu kutokana na ucheleweshaji wa ulipaji wa kodi.

Philipo Eliamini ni Afisa elimu na Huduma kwa mlipa kodi kutoka mamlaka ya mapato Tanzania TRA Mkoani hapa ,akizungumza leo na Maisha fm kupitia kipindi cha Maisha Breakfast amewakumbusha wafanya biashara kukamilisha zoezi la ulipaji kodi kwani  mwisho wakulipa kodi ya awamu ya tatu ni Tarehe 30,mwezi septemba,2020.

‘’Ndugu wafanyabiashara kama tunavyofahamu sheria yetu ya mapato ianamtaka kila mfanyabiashara anayepata kipato au kila mtu anayepata kipato kulipa kodi ya mapato kila mwaka na kama mtakumbuka kila mwaka huwa tunautaratibu wa kufanya makadirio ya kodi na mara nyingi makadirio haya kwa wale wafanyabiashara hutumia mwaka wa kalenda kwa maana ya januari mpaka disemba hufanyika kuanzia mwezi januari mpaka machi na baada ya kufanya makadirio haya huwa tunatoa awamu nne za ulipaji wa mapato awamu ya kwanza huwa ni mwezi wa tatu ,awamu ya pili mwezi wa sita na awamu ya tatu huwa ni mwezi septemba na mwisho wa nne huwa ni mwezi disemba ‘’Philipo

Aidha philipo amewataka wafanyabiashara hayo kulipa kodi kwa wakati ili serikali iweze kutekeleza majukumu yake katika kuboresha miundomninu kama vile elimu,afya pamoja na ulinzi na usalama,huku akiongeza kuwa kushindwa kulipa kodi kwa wakati kunaweza kusababisha madhara kwa serikali na wafanyabiashara wenyewe.

‘’unapochelewa kulipa kodi au usipo lipa kodi kimsingi kuna madhara mbalimbali kuna madhari kwako wewe mfanyabiashara lakini pia kwa serikali lakini pia kuna madhari kwa jamii inayokuzunguka’’ Philipo

Sanjari na hayo Afisa huyo amehitimisha kwa kuwakumbusha waajiri kuwasilisha mapema kodi wanazokata kutoka kwa wafanyakazi wao,hivyo amewaasa kodi hizo ziwasilishwe mapema kabla ya tarehe 7, ya mwezi mwingine wa malipo kwa kuwa ni takwa la kisheria.

‘’TRA inamtaka kila mwajiri anayezuia kodi hiyo si zaidi ya tarehe saba ya kila mwezi unaofuata kwa mfano kodi za mishahara ya mwezi tisa ziwasilishwa si zaidi ya tarehe 7 ya mwezi wa kumi lakini sasa tunasema kwanini usubiri mpaka tarehe saba kama wewe umeshalipa mshahara kuna baadhi ya waajiri wanalipa mshahara mapena tarehe 20 ,25,26  sasa kimsingi zile kodi umewakata wafanyakazi sasa kama umeshazikata tunakusihi uziwasilishe mapema’’Philipo

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.