TAASISI YA HABARI DEVELOPMENT ASSOCIATION YALAANI MATAMSHI YA UCHOCHEZI YANAYOTOLEWA NA BAADHI YA WAGOMBEA KATIKA KAMPENI

 



Mratibu wa Taasisi ya Habari Development Association Hamis Shime akizungumza na waandishi wa Habari katika Mkutano uliofanyika Jijini Tanga. 


Na Jackline Kuwanda, Tanga

Taasisi ya Habari Development Association imelaani vikali matamshi ya uchochezi yanayotolewa na Baadhi ya wagombea katika kampeni zao.

Kauli hiyo imetolewa Jijini Tanga na Mratibu wa Taasisi hiyo  Hamis Shime wakati akizungumza na waandishi wa Habari Jijini humo.

‘’ Mfano maneno ya mgombea wa Urais Chadema Tundulisu akiwa kwenye kampeni katika Mikoa mbalimbali Geita,Mara,Mwanza ,Bukoba,Songwe na wilaya Tarime maneno kama utawala huu ni kizarimu mara oh nimeshinda uchaguzi mkuu mara tuko kwenye utawala wa hovyo mara tumetawaliwa na kiongozi muovu jambo ambalo ni baya na ni matusi kwa watanzania watanzania si wote wenye ushabiki na vyama hivyo ’’ Amesema Shime

Amesema linapokuja suala la kumtukana Rais aliyepo madarakani na yupo kwenye kampeni siyo kitu kizuri kwani watanzania walio wengi wanahitaji sera na maono ya nini yatafanyika katika kipindi cha miaka mitano.

‘’tunalaani matamshi ya aina hiyo na tunaipongeza hatua iliyochukuliwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi NEC ya kumuita tundulisu kwenye kamati ya Taifa ya maadili’’ Amesema Shime

Katika hatua nyingine Shime ametoa wito kwa vijana  maeneo yote nchini kutotumika na wanasiasa badala yake kuendelea na majukumu yao kama kawaida na siku ya kwenda kupiga kura basi waende kupiga kwa utulivu.

‘’kwa kuwa wako baadhi ya wanasiasa wanataka kutuharibia nchi yetu ambayo imetulia ina amani watu wanafanya shughuli zao vizuri na hakuna bughuza yeyote ile,vijana tutulie tufuate maagizo ya viongozi wetu ‘’

Kwa upande wake makamu mwenyekiti Taasisi hiyo  Issa Omary Chambo amesema kwa sasa vijana wanajitambua kwani hujua ni mgombea yupi anayeeleza sera za kimaendeleo na ni yupi mgombea yupi anaye eneza chuki katika nchi.

‘’kwa hiyo kupitia nyinyi ule ujumbe utakuwa ni rahisi kuwafikia hawa vijana sidhani kama wapo vijana ambao wanaweza wakatumika vibaya’’ Amesema Chambo

Naye Benald James Katibu Taasisi hiyo amesema nchi ya Tanzania ni nchi ambayo haijazoea vurugu matamshi ya kuwagawa watanzania hajiazoeleka hivyo ni mbaya kwa mgombea yeyote Yule kuacha kunadi sera za chama chake na ilani yake na kuanza kunadi matamshi ambayo yanaweza kuhatarisha usalama wa  nchi.



Benald James Katibu wa Taasisi ya Habari Developement Association akizungumza katka mkutano wa waandishi wa Habari uliofanyika Jijini Tanga


‘’Tunaimani na tunaioyomba tume na vyombo vingine ambavyo vinasimamia uchaguzi visisite wala kumuonea huruma mtu yeyote kumchukulia hatua ikiwezekana hata kuzuia asifanye kampeni’’ Amesema James

Hatahivyo wamesema wanaamini uchaguzi wa Mwaka huu utafanyika kwa amani na zile changamoto ambazo wananchi wanazipitia zitatatuliwa .

Mwisho

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.