Nchini Tanzania kila mwaka takribani watoto elfu 11,000 huzaliwa na sikoseli-Kiologwe

 


Na Jackline Kuwanda, Dodoma.

Kwa mujibu wa Takwimu zilizotolewa na shirika la Afya Duniani WHO 2015 lilitoa taarifa inayoonesha kuwa kila siku Duniani zaidi ya watoto elfu moja (1000) huzaliwa na sikoseli .

Huku kwa nchi ya Tanzania takwimu zikionesha kuwa kila mwaka Takribani watoto elfu kumi na moja (11,000) huzaliwa na ugonjwa wa sikoseli.

Hayo yamesemwa leo jijini Dodoma na Mkurugenzi Msaidizi anayeshughulika na magonjwa yasiyo ya kuambukiza Dkt James kiologwe kwa niaba ya Mganga Mkuu wa Serikali Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii ,Jinsia , Wazee na Watoto Prof  Abel Makubi wakati akihitimisha mwezi wa kuelimisha jamii juu ya ugonjwa wa sikoseli ulioanza Septemba 1 na kumalizika septemba 30,2020.

‘’ Takwimu hizi zinaifanya Tanzania kuwa nchi ya nne Duniani kuwa na wingi wa ugonjwa wa sikoseli ikiongozwa na Nigeria ambapo watoto ishirini hadi thelathini kati ya elfu moja wanazaliwa kila mwaka  wakiwa na sikoseli’’ Amesema

Amesema hadi sasa Tanzania ina takribani zaidi ya wagonjwa laki mbili wa sikoseli wanaotambulika kwenye vituo vya kutolea huduma za Afya huku akisema takwimu zinaonesha kuwa kati ya watanzania mia moja miongoni mwao 15-20 wanavinasaba vya ugonjwa huo hivyo wanauwezekanao wa kupata watoto wenye ugonjwa wa sikoseli  iwapo watakuwa na wenza wenye vinasaba vya sikoseli.

‘’tafiti mbalimbali zilizofanywa hapa nchini zinaonesha kwamba takribani watoto saba kati ya mia moja wenye umri wa miaka mitano hufariki kutokana na ugonjwa wa sikoseli’’ Amesema

Kwa upande wake Daktari Bingwa wa Magonjwa ya ndani kutoka Hospitali ya Muhimbili Jijini Dar es salaam Dkt Elisha Osati amesema katika kipindi chote cha mwezi wa tisa wameweza kutoa elimu kwa jamii juu ya ugonjwa wa sikoseli lakini inaonekana kuwa bado kwa nchi ya Tanzania kunaelewa mdogo kuhusiana na ugonjwa huo.

‘’nchi yetu bado kuna uelewa mdogo kuhusiana na ugonjwa huu katika kipindi cha mwezi wa tisa tumejitahidi kufanya mambo megni ikiwemo kutoa elimu kwa jamii kuufahamu zaidi ugonjwa huu na njia pekee ya mtu kujikinga asipate sikoseli ni kujiepusha kuingia kwenye mahusiano na mtu mwenye vinasaba vya sikoseli’’ Amesema

Zuhura Makuka ni mama mwenye mtoto mwenye ugonjwa wa sikoseli amesema watoto wengi wana ugonjwa huo lakani wazazi hawafahamu kama watoto wana maradhi hayo huku akigusia kuwa kuna hali ya unyanyapaa kwa watoto wenye ugonjwa huo na wapo pia ambao huusisha ugonjwa huo na imani za kishirikina.

‘’ukitembelea vituo vya kutolea huduma za afya ukienda wodini asilimia kubwa ya watoto wana sikoseli ugonjwa huu lakini haufahamiki na unyanyapaa bado ni mkubwa wanaamini kuwa mtoto anapozaliwa na ugonjwa huu basi amerogwa’’ Amesema

Mwingine wa wakina mama  ambaye ana mtoto  mwenye ugonjwa wa sikoseli anaeleza hali ilivyokuwa wakati bado hajafahamu kuwa mtoto wake ana ugonjwa huo.

‘’ nilianza kuona mwanangu ana kama kiuvimbe kwenye mkono tukakaa tena siku tatu nikaona tena mkono mwingine ukaanza kuvimba alikuwa analia sana  baada ya kwenda kituo cha afya cha makole  wakanambia mwanao hana damu wakanambia niende hospitali ya rufaa ya mkoa wa Dodoma baada ya kwenda walimpima wakaniambia mtoto wako ana ugonjwa wa sikoseli’’ Amesema

Ugonjwa wa Sikoseli yaani selimundu hutokana na kurithi kutoka kwa Wazazi wawili yaani Baba .

Hitimisho la mwezi wa kuelimisha jamii juu ya ugonjwa wa sikoseli ulianza septemba 1 hadi 30 umekwenda sambamba na kauli mbiu isemayo ‘’Ijue Sikoseli,Epuka Unyanyapaa’’

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.