Na. Mwandishi Wetu,
Mamlaka
ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) imetangaza nauli za treni ya abiria
itakayofanya safari zake kutoka Moshi mjini hadi Arusha na kurudi Moshi.
Akizungumza na waandishi wa habari Mkoani Arusha leo tarehe 29 Septemba, 2020,
Mkurugenzi Mkuu wa LATRA, Gilliard Ngewe amesema nauli hizo zimetangazwa
kufuatia Shirika la Reli Nchini (TRC) kuwasilisha maombi ya nauli hizo, ambapo
LATRA ilifanya mikutano ya kupokea maoni ya wadau, kisha kufanya uchambuzi wa
maoni hayo pamoja na kuchambua mchanganuo uliowasilishwa na TRC.
Kwa
mujibu wa kifungu cha 21 (2) (b) cha Sheria ya LATRA namba 3 ya 2019, baada ya
mchakato wa uchambuzi kukamilika, Bodi ya Wakurugenzi ya LATRA imeidhinisha
nauli hizo na kuainisha nauli zitakazotumika kwa usafiri wa treni ndani ya mikoa
hiyo na nje ya mikoa kama inavyoonekana katika jedwali.
Nauli
zilizoidhinishwa na LATRA zikionesha mchanganuo wa vituo vya ndani nan je ya
mikoa husika
|
KUTOKA
MOSHI KWENDA |
Umbali
(KM) |
NAULI
KWA MADARAJA HUSIKA (SHS): |
|
Daraja
la tatu |
Pili
kukaa |
|||
1 |
RUNDUGAI |
22 |
1,000 |
1,500 |
2 |
KIKULETWA |
31 |
1,000 |
1,500 |
3 |
KIA |
37 |
1,000 |
1,500 |
4 |
USA RIVER |
62 |
1,500 |
2,000 |
5 |
TENGERU |
65 |
1,500 |
2,000 |
6 |
CHEKERENI |
75 |
1,500 |
2,000 |
7 |
NJIRO |
82 |
1,500 |
2,000 |
8 |
ARUSHA |
86 |
1,500 |
2,000 |
|
KUTOKA
ARUSHA KWENDA |
Umbali
(KM) |
NAULI
KWA MADARAJA HUSIKA (SHS): |
|
Daraja
la tatu |
Pili
kukaa |
|||
1 |
NJIRO |
4 |
1,000 |
1,500 |
2 |
CHEKERENI |
11 |
1,000 |
1,500 |
3 |
TENGERU |
21 |
1,000 |
1,500 |
4 |
USA RIVER |
24 |
1,000 |
1,500 |
5 |
KIA |
49 |
1,500 |
2,000 |
6 |
KIKULETWA |
55 |
1,500 |
2,000 |
7 |
RUNDUGAI |
64 |
1,500 |
2,000 |
8 |
MOSHI |
86 |
1,500 |
2,000 |
Nauli
za wanafunzi kutoka mwanzo hadi mwisho wa safari ni Sh. 300.00 kwa daraja la
tatu, na Sh 400.00 kwa daraja la pili kukaa.
Mkurugenzi Mkuu LATRA Gilliard Ngewe akimkabidhi Henry Machoke, Mkurugenzi wa Maendeleo ya Biashara TRC andiko la nauli zilizoidhinishwa
Wakati
huo huo, LATRA imeiagiza TRC kutekeleza masuala mbali mbali ikiwa ni pamoja na
kutoa elimu ya usalama kwa wadau husika, kutumia mfumo wa tiketi za
kielektroniki, kutoa ratiba za safari kwa umma, kutekeleza hatua za usalama
kudhibiti msongamano wa abiria, kuboresha miundombinu na huduma za kijamii,
kuweka kitengo cha huduma kwa wateja na kutangaza nauli zilizoidhinishwa katika
vyombo mbalimbali vya habari ili ziwafikie wadau wengi zaidi.
Comments
Post a Comment