Zoran Zaev aidhinishwa kuwa Waziri Mkuu wa Macedonia



Wabunge wa Macedonia Kaskazini wamemuidhinisha Zoran Zaev kuwa waziri mkuu baada ya kumpigia kura 62 dhidi ya 51 kuchukua wadhifa huo. Zaev anatarajiwa kurejea ofisini baada ya kuondoka Januari, kufuatia mpango uliofikiwa mwezi huu kati ya chama chake cha Social Democratic - SDSM na Democratic Union for Integrations - DUI, chama kikubwa kinachoiwakilisha jamii ya Waalbania. 

Ratiba ya Zaev ni pamoja na kumteuwa waziri mkuu mwenye asili ya Kialbania mwishoni mwa muhula wa serikali.

Kura hiyo imepigwa baada ya saa nyingi za mdahalo jana. Itakuwa mara ya kwanza tangu nchi hiyo iliyojitenga kutoka Yugoslavia ya zamani mwaka wa 1991 kuwa na waziri mkuu mwenye asili ya Kialbania. Waalbania wamekuwa wakishinikiza kupewa haki zaidi tangu nchi hiyo ilipopata uhuru.

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.