CHAMWINO,DODOMA.
MKURUGENZI Mtendaji wa Shirika lisilo la kiserikali la AFNET Sara Mwaga,amewaomba wananchi wa kijiji cha Kawawa wilaya ya Chamwino ambao wana vitambulisho vya kupiga kura kuvitendea haki kwa kuwapigia viongozi watakaoleta maendeleo kwa masilahi ya watanzania wote.
Aidha amewahamasisha wananchi
hao kuhakikisha hawapotezi haki yao kutokana na kudanganyika kwa kununuliwa
chakula,vitenge,fedha na kanga,kwa kuwa wanaweza kujikuta ikiwagharimu kwa
kuwachagua viongozi mabomu wenye kujali maslahi yao.
Mwaga alisema hayo alipokuwa
akizungumza na wananchi wa kijiji hao walioshiriki kwenye maombi maalumu
kuombea Taifa na uchaguzi mkuu utakaofanyika mwaka huu yaliyoandaliwa na kanisa
la Kipentekost la Sayuni Tanzania lililopo kijiji cha Kawawa kata ya Msanga
wilayani Chamwino.
Alisema wananchi wenye
vitambulisho hivyo vya kupiga kura wanatakiwa kutumia haki ya kimsingi ya
kuwachagua viongozi watakaofanisha kutatua changamoto za watanzania bila kujali
watu watakaowatumikia wanatoka kwenye chama kipi.
Mkurugenzi huyo amewaomba
wananchi hao walioshiriki kwenye maombi hayo ambao wana vitambulisho vya
kupigia kura kuacha tabia ya kubweteka majumbani siku ya upigaji,badala yake
wajitokeza watumie haki ya msingi ya kuwapata viongozi wanaowataka wao wenyewe.
“Haipendezi mwananchi una
kitambulisho cha mpiga kura halfu ukakaanacho nyumbani siku ya upigaji
kura,ninawaomba mjitokeze kwa wingi ili mtumie haki yenu ya kisingi ya
kuwachagua viongozi mnaowataka wenyewe na msisubiri kuchaguliwa na
wengine”alisema.
Kwa upande wake Mchungaji
kiongozi Jonas Kabia wa kanisa hilo la Sayuni,alisema kuwa kuelekea uchaguzi
mkuu wa mwaka huu Taifa la Tanzania halitegemei kuwapata viongozi watakaowagawa
watanzania kutokana na itikadi za vyama vyao.
Alisema watanzania mategemeo yao
makubwa kwenye uchaguzi huu wa mwaka 2020 ni kuona wanatumia demokrasia
ya haki na huru katika kuwachagua viongozi wanaowania nafasi hizo ikiwemo ya
urais,ubunge na udiwani.
Hata hivyo alisema kuwa malengo
ya maombi hayo maalumu ni pamoja kumumba Mungu ili awawezeshe viongozi
watakaochaguliwa kwenye uchaguzi huu wa 2020 waweze kutekeleza ahadi ambazo
watakazozisema kupitia sera za vyama vyao.
MWISHO.
Comments
Post a Comment