JPM KUJENGA UWANJA MKUBWA WA MICHEZO JIJI LA DODOMA

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

Mgombea uras kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi, Dkt. John Magufuli kujenga uwanja mkubwa wa michezo Dodoma utakaoweza kubeba wananchi wengi zaidi kwa wakati mmoja.

Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM, Dkt. John Magufuli


Dkt. Magufuli ametoa kauli hiyo katika hotuba yake ya uzinduzi wa kampeni ya kuwania urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma leo.

“Leo Dodoma imefurika, uwanja wa Jamhuri umejaa, lakini hata kule nje nako kumejaa. Hii inanipa changamoto kuwa nitakapochaguliwa kuwa Rais ni lazima nijenge uwanja mkubwa kuliko uliopo na hii itakuwa ndiyo kazi yangu ya kwanza. Dodoma ni Jiji, na leo mmefunga kazi, asanteni sana wana Dodoma. Hii inadhihirisha wazi kuwa hapa ni makao makuu ya nchi” alisema Dkt. Magufuli.

Aidha, aliwataka watanzania kuendelea kumuomba Mungu ili azidi kuliongoza na kulisimamia Taifa la Tanzania liendelee kuwa na amani na umoja katika kipindi cha uchaguzi mkuu na baada ya uchaguzi mkuu.

Akimkaribisha mgombea urais kwa tiketi ya CCM, mgombea mwenza wa chama hicho, Mama Samia Suluhu Hassan, alisema kuwa serikali chini ya CCM imetekeleza kwa kishindo Ilani ya uchaguzi ya chama hicho. “Ndugu wananchi niseme, katika kipindi cha miaka mitano iliyopita tumeweza kutekeleza kwa kishindo na tumeweza…Twende tukasonge mbele katika kampeni kwa heshima na kuomba kura kwa wananchi. Tukafanye kampeni kwa amani na kupiga kura kwa kishindo, tupate maeneldeleo ya kisiasa, kiuchumi na kijamii” alisema Mama Samia.

Chama cha Mapinduzi kimezindua kampeni kuelekea uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani katika uwanja wa Jamhuri jijini hap ana zitaendelea nchi nzima kwa takribani miezi miwili.

MWISHO

 

 

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.