WANAFUNZI ZAIDI YA 20 SHULE YA SEKONDARI KATUMBA WILAYANI MPANDA WAFUKUZWA SHULE,WAZAZI WASHINDWA KUMUDU MICHANGO





Na. Mwandishi Wetu, MPANDA
Wanafunzi zaidi ya 20 wa Kidato cha nne Katika shule ya Sekondari Katumba iliyopo Wilaya ya Mpanda Mkoani Katavi wamefukuzwa shuleni na kupewa adhabu ya kufyatua tofari 300 kila mmoja ikiwa ni adhabu ya kutoishi Bwenini kama mkakati wa shule hiyo.

Mpanda Redio FM imezungumza na Wazazi na walezi wa baadhi ya wanafunzi hao ambao wamesema wameshindwa kumudu michango ya chakula inayofikia kiasi cha elfu 65 na kwamba adhabu hiyo imetolewa wakati wanafunzi wengine wakiendelea na mitihani ya kujipima .

Tumemtafuta Mkuu wa shule hiyo bila mafanikio , Lakini Mpanda Redio fm inafanya jitihada za kumtafuta Mkurugenzi wa Halmashauri ya Nsimbo pia .

Hivi karibuni Waziri Mkuu wa Tanzania akiwa mkoani Katavi kwajili uzinduzi wa ujunzi wa Bandari ya Kalema aliagiza wakuu wa shule kuacha kufukuza wanafunzi kwaajili ya michango badala yake waache wanafunzi waendelee na Masomo.

Chanzo Mpanda Redio FM

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.