Na.
Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
Shirika la Reli Tanzania-TRC limesema kuwa
limeazimia kushirikiana kwa ukaribu na asasi za serikali na binafsi ili
kuhakikisha jamii inayoishi pembezoni mwa reli zinafaidika na ujio wa miradi
inayisimamiwa na TRC wakati wa ujenzi, na mara baada ya ujenzi na
uboreshaji wa reli ya kati inayotoka mkoa wa dar es salaam hadi isaka.
Akizungumza jana jijini Dar es
salaam mara baada ya TRC na Taasisi hizo kusaini mikataba ya utekelezaji
wa mikakati mbalimbali ili kuboresha maisha ya jamii zinazoishi pembezoni mwa
reli, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa shirika hilo, Amina Lumuli amesema
mikakati ya kuboresha jamii hizo imetokana na matokeo ya kazi kubwa inayofanywa
na serikali kwa kufanya maamuzi ya kuimarisha sekta ya miundombinu ya reli
nchini ikiwa ni pamoja na kujenga reli yenye kiwango cha kimataifa -SGR,
Kuboresha reli ya kati pamoja na kufufua njia mbalimbali za reli.
Aidha, amebainisha
kuwa shirika la reli linatambua umuhimu na mchango unaotolewa na taasisi
binafsi na za serikali kwa jamii hivyo TRC itaendelea kuongeza nguvu na
ushirikiano kwa taasisi hizo ili kuleta matokeo chanya katika utekelezaji wa
miradi nchini.
Kwa upande wake Meneja miradi
wa ujenzi wa Reli ya SGR anayehusika na ujenzi kutoka Dar es salaam mpaka
Morogoro Machibia Masanja amesema kuwa uwepo wa ujenzi wa mradi huo
utakuwa na manufaa kuanzia ujenzi wake mpaka kuendelea kutumika
MWISHO
Comments
Post a Comment