Na. Mwandishi Wetu, SHINYANGA
Tanzania kwa sasa ni moja ya nchi bora barani Afrika
ambayo imewekeza katika miundombinu ya Sekta ya Afya kwa kiwango kikubwa ikiwa
ni moja ya mafanikio makubwa kwa serikali ya wamu ya tano kwa sasa.
Mkurugenzi wa Kinga kutoka Wizara ya Afya, Dkt. Leornad
Subi amesema hayo jana alipofika Wilayani Kahama kufanya ukaguzi shirikishi na
kujionea miundombinu mpya ya Sekta ya Afya Wilayani Kahama.
Dkt. Subi alitaja lengo la Wizara ya Afya
kufanya ukaguzi katika miundombinu ya Afya ni kuona huduma zinazotolewa katika
sekta ya Afya inakizi viwango kwa lengo la kutoa huduma bora na za uhakika kwa
wananchi.
Aidha, Dkt. Subi
aliongeza kuwa lengo kubwa la serikali ni kuona kuna ufanisi mkubwa wa huduma
zianzotolewa katika miundombinu hiyo ikiwa ni pamoja na kuongeza vifaa tiba
vitakavyowawezesha wahudumu wa Afya kutoa huduma zenye ubora ili kuhimarisha
Afya za wananchi ikiwemo kupunguza vifo vya mama na mtoto.
Dkt. Subi ameongeza kuwa ukaguzi wake
katika hospitali ya Mji Kahama amegundua kuwa kuna mapungufu ya kiutendaji
ambayo ni kutoweka vizuri kumbukumbu katika vitabu vya Mtua kwakuwa kuna
masuala ya msingi ambayo wahudumu wa Afya wameonekana kutoweka kumbukumbu zake
kama inavyotakiwa.
Pamoja na kubaini mapungufu hayo, Dkt. Subi
amelekeza wataalam wa Afya kuhakikisha wanafanya ukaguzi wa madawa mara kwa
mara na kuwasilisha taarifa ya ukaguzi huo kwa Mkurugenzi ili kuweza
kukabiliana kwa wakati na upungufu wa vifaa tiba katika hospitali wilayani
Kahama.
Aidha, ameongeza
kuwa Serikali imekuwa ikitumia rasimali nyingi kuhakikisha kuna upatikanaji wa
dawa za kutosha lakini pia kumekuwepo upotevu wa dawa unaosababishwa na
baadhi ya watumishi wasio kuwa waaminifu kwa kutofuata mifumo iliyopo au kuweka
taarifa vizuri hivyo kuwataka kufanya ukaguzi wa mara kwa mara na kuweka sawa
taarifa ya matumizi ya vifaa tiba.
Dkt. Subi ameongeza kuwa kimsingi Idara
yake inaangazia sana utoaji elimu ya Afya kwa wananchi kwani elimu ya Afya ndio
msingi wa huduma za kinga hapa Nchini akitolea mfano Wilaya ya Kahama kuwa na
idadi kubwa ya maambukizi ya ugonjwa wa UKIMWI.
“Wilaya ya Kahama ina jumla ya wagonjwa 15,000 wanaotumia dawa za
kupunguza makali ya UKIMWI idadi hii ni kubwa sana lakini tukitoa elimu ya
UKIMWI idadi hii inaweza kupungua kwa kiasi kikubwa sana na kuokoa fedha nyingi
za serikali zinazotumika kununua dawa za ARV.’’ aliongeza
Mkurugenzi Idara ya Kinga Dkt. Leornard Subi.
Pamoja na masuala mengine
yanayoshughulikiwa na idara ya Kinga ya Wizara ya Afya, Dkt. Subi
ameongeza kuwa Idara yake pia inashughulikia masuala ya lishe suala ambalo
kimsingi ni la utoaji elimu kwa umma na kuoji kuwa kwanini bado kuna udumavu
katika jamii zetu kwani Tanzania ni Nchi inayozalisha Chakula cha kutosha na
kusema kuwa sio tu watoto wana udumavu wa kimo pia wanachangamoto ya udumavu wa
akili.
Naye Mkurugenzi wa Mji wa Kahama, Bw. Anderson
Msumba amesema kuwa kwa upande wake ameona mapungufu yaliyobainishwa na ukaguzi
shirikishi na kuhaidi kuyafanyia kazi kwa kipindi kifupi yale amabayo hayaitaji
fedha laikini pia yale yanayoitaji rasilimali fedha atayafanyia kazi kabla ya
Desemba Mwaka huu.
Idara ya Kinga ya Wizara ya Afya inaendelea
na kazi ya ukaguzi wa miundombinu ya Hospitali kwa mikoa ya Kanda ya Ziwa
ambayo ni Shinyanga, Mwanza, Simiyu, Geita, Mara na Kagera.
MWISHO
Comments
Post a Comment