MAOFISA MIPANGO MIJI WATAKIWA KUACHA TABIA YA KUACHIA KAMPUNI BINAFSI KURASIMISHA ARDHI KATIKA MAENEO BILA KUWA NA USIMAMIZI WAO




Na. Mwandishi Wetu, DODOMA
Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Doroth Mwanyika amewataja maofisa mipango miji kuwa chanzo cha ujenzi holela ambao umekuwa ukijitokeza katika maeneo mbalimbali kwani hawatekelezi majukumu yao ipasavyo.

Akizungumza jijini hapa jana kwenye mafunzo ya siku mbili ya maofisa mipango miji wa Mikoa na Makao makuu ya Wizara ya Ardhi, kwa niaba ya Katibu Mkuuu, Mkurugenzi wa Sera na Mipango wizara hiyo, Ezekiel Mpanda amesema maofisa hao wamekuwa wakilalamikiwa kila sehemu kutokana na utendaji wao wa kazi.

Mpanda amesema maofisa hao hawatoi elimu kwa wananchi ili wajue sheria za adhi na kawaacha wajenge holela, hali ambayo inasababisha wengi kubomolewa nyuma zao na kuingia hasara.
Hata hivyo amewataka maofisi hao kuacha tabia ya kuwaachia kazi kampuni binafsi kurasimisha maeneo bila kuwa na usimamizi wao kwani baadhi yao wamekuwa wakishindwa kukamilisha kazi waliyopewa kwa wakati.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Usajili wa Wataalam wa Mipango Miji, Prof. Wilbard Kombe amesema Maofisa hao licha ya kazi wanazozifanya lakini baadhi yao wamekuwa si waaminifu kwani wanafanyakazi na kampuni ambazo hazijasajiliwa.

Akizungumzia utafiti walioufanya hivi karibuni kuhusu Mipango Miji, mkuu wa Shule kuu ya Mipango Miji katika Chuo Kikuu cha Ardhi, Dk Ally Namangaya amesema utafiti huo ulilenga kujua kwanini utekelezaji wa mipango miji ni mdogo katika maeneo mbalimbali nchini huku Ofisa Mipango Miji mkoani Geita, Oscar Yohana akieleleza jisni watakavyokabiliana na changamoto hizo.

MWISHO




Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.