JESHI LA MAGEREZA DODOMA LALEGEZA MASHARTI KATAZO LA KUTOTEMBELEA WAFUNGWA

Na. Mwandishi Wetu, DODOMA
KUTOKANA na kupungua kwa hali ya maambukizi ya ugonjwa wa Covid-19 nchini Jeshi la Magereza limelegeza masharti ya katazo la kutokutembelea wafungwa na mahabusu ambapo kuanzia Agosti 1 mwaka huu huduma ya kutembelea wafungwa/mahabusu kwa huduma mbalimbali magerezani zimerejeshwa.
SSP Amina Kavirondo
Akizungumza na waandishi wa Habari leo Jijini Dodoma Msemaji wa Jeshi la Magereza, SSP Amina Kavirondo amesema kuwa kufuatia kuripotiwa uwepo wa ugonjwa wa Corona nchini jeshi la magereza lilisitisha huduma zote za kutembelea wafungwa na mahabusu ikiwemo huduma za kupelekewa chakula.

Hatua hii imekuja baada ya kushuka kwa kasi ya maambukizi Tanzania kwa kiasi cha kuridhisha na kwa kuzingatia tamko la Rais John Magufuli la kuzitaka taasisi mbalimbali za serikali kurejea katika shughuli za awali za utendaji kazi” amesema.

Amesema kuwa Jeshi la Magereza linawataka wageni wote pamoja na kuzingatia sheria,kanuni na miongozo ya jeshi na wizara ya afya wakati wa upokeaji wa huduma hiyo.

Wakati huohuo, alisema kuwa wageni watatakiwa kuzingatia mambo muhimu yafuatayo,mfungwa/mahabusu atatembelewa na ndugu wasiozidi wawili tu kati ya jumamosi au jumapili,mazungumzo yatatakiwa yasizidi dakika tano,na wenye vibali vya kuleta chakula italazimika kuletwa na mtu mmoja tu.

“Mambo mengine ni pamoja na wageni wote wavae barakoa na kunawa mikono kwa maji tiririka na sabuni wanapoingia eneo la Gereza na wanapongia gerezani,kuwa umbali wa mita moja kati ya mfungwa/mahabusu na mgeni  lazima uzingatiwe na mazungumzo ya kisheria kati ya wakili na mteja wake yasizidi saa moja” alisema Kavirondo.


MWISHO

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.