CHAMA CHA ADC CHATOA FOMU ZA UBUNGE,WAWAKILISHI NA MADIWANI WENGI WAKIWA NI WANAWAKE

Na. Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
Chama cha Siasa cha Aliance for Democratic Change (ADC) kimesema mpaka sasa kimetoa fomu za Ubunge 36, wawakilishi 32, pamoja na Madiwani 76 mkoa wa Dar es salaam wengi wakiwa ni wanawake wanaotaraji kupeperusha bendera ya chama hicho katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba mwaka huu.

Kauli hiyo imetolewa leo Jijini Dar es salaam na Naibu Katibu wa Chama hicho, Queen Cuthbeti Sendiga wakati akifanya mahojiano maalum na kituo hiki akieleza namna wanavyoendesha mchakato wa uchukuaji wa fomu za wagombea nafasi mbalimbali za uongozi kupitia chama hicho.

Naibu Katibu huyo wa ADC ambaye pia ndiye Mgombea Urais wa Tanzania Bara kwa chama hicho amesema chama chao kimepata muamko wa wanawake wengi kujitokeza kuchukua fomu ili kupata nafasi ya kugombea Ubunge pamoja na Udiwani kupitia chama hicho.

Aidha, ameziomba Taasisi zote zinazojihusisha na kuwawezesha wakina mama kusimamia katika uongozi ni vyema zikaonyesha mchango katika kuwapa mbinu na jitihada wanawake katika Kupambana kwenye uchaguzi ili kuibuka vinara wa ushindi.


Naibu katika huyo amewahamasisha watanzania kusimama vyema katika kuilinda na kuitunza amani ya nchi ili uchaguzi huo uweze kufanyika kwa utulivu na kumpata kiongozi bora.

Hata hivyo Chama hicho cha Aliance Democratic Change ADC kimesha fanya uchaguzi na kuwateua viongozi wakubwa wa nchi Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano na Mwenza pamoja na mgombea wa Urais serikali ya mapinduzi ya Zanzibar.


MWISHO

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.