Wanafunzi Shule ya Msingi Dodoma Mlimani waeleza Furaha yao Baada ya kurejea Shuleni,Tutasoma kwa Bidii,Tuliwakumbuka sana Walimu wetu, Muda wa kucheza haupo tena
![]() |
Wanafunzi wa Darasa la saba wa Shule ya Msingi Dodoma Mlimani wakinyoosha mikono kwaajili ya kujibu maswali yaliyokuwa yakiulizwa na Mwalimu aliyekuwa akiwafundisha Darasani |
Na Jackline Kuwanda, Dodoma.
Wanafunzi
wa shule ya Msingi Dodoma Mlimani iliyopo Mkoani Dodoma wameonesha hali ya
furaha kwa kurejea tena shuleni baada ya kukaa nyumbani kwa takribani miezi
mitatu kutokana na Ugonjwa wa Homa kali ya Mapafu inayosababishwa na Virusi vya
Corona (COVID-19).
Janga
la Corona lilichangia kwa kiasi kikubwa kukwamisha kuendelea kwa shughuli
mbalimbali hapa Nchini ikiwemo pia Vyuo kufungwa, Shule za Awali ,Msingi na Sekondari
nazo zilifunguwa lengo lilikuwa ni kuepusha kuenea kwa maambukizi ya ugonjwa
huu.
Jumanne
June 16,2020 wakati akitoa hotuba yake ya kuvunja Bunge la 11, Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli alitangaza rasmi kufunguliwa
kwa shule zote zilizofungwa kutokana na ugonjwa huo na June 29 ndiyo ilikuwa
tarehe rasmi ya wanafunzi kurejea shuleni.
Dodoma
News Blog ilitembelea shule hiyo ili kujionesha hali halisi baada ya wanafunzi
pamoja na walimu kurejea shuleni .
‘’Tuliwakumbuka sana walimu wetu kipindi
tulichokuwa nyumbani,muda mwingi umepotea, kwa sasa tumerejea shuleni sio muda wa kucheza tena, tutasoma kwa bidii
na tutafaulu’’
Wanafunzi
wa Darasa la Saba katika shule hiyo ambao wanatarajia kufanya mitihani yao ya
kuhitimu elimu ya msingi hivi karibuni wanaeleza namna ilivyokuwa kipindi
walipokuwa nyumani na sasa wamerejea shuleni .
Hemedy
shabani ambaye anasoma Darasa la saba katika shule hiyo alisema anafuraha sana
kurejea shuleni lakini katika kipindi chote alichokuwa nyumbani alikuwa
akijisomea kwenye madaftari yake lakini pia kupitia Runinga.
‘’najua
kuwa ninatarajia kufanya mtihani wangu wa kuhitumu elimu ya msingi nitasoma kwa
bidii kwakuwa muda tuliyopoteza ni mwingi sana sasa hivi sio muda wa kucheza’’
Alisema Hemed
Grace
Steven alisema wakati yuko nyumbani alikuwa akijifunza masomo ya Darasa la saba
kupitia Radio kwani alikuwa akijitahidi
kusikiliza kwa umakini na alikuwa akiwaelewa walimu ambao walikuwa
wakifundisha.
‘’kazi
walizokuwa wakitupa nilikuwa nafanya na majaribi mengine nilikuwa nafanya
kupitia mitihani yangu ya zamani niliwakumbuka walimu wangu jinsi walivyokuwa
wanatufundisha’’ Alisema Grace
Naye
Elizabelth David ambaye pia yuko Darasa la saba alisema amerejea tena shuleni
hivyo atasoma kwa bidii ili aweze kufaulu mitihani yake vizuri.
‘’tuliwakumbuka
sana walimu wetu,Tumekaa nyumbani muda mrefu na hivi sasa tumerejea shuleni
nitasoma kwa bidii,nakumbuka wakati niko nyumbani nilikuwa na muda wa kujisomea
kupitia madaftari yangu na kupitia runinga kwenye Darasa huru’’ Alisema Elizabelth
Nao
wanafunzi wa Darasa la nne katika shule hiyo walisema kuwa wanajisikia vizuri
kurejea tena shuleni na wamejipanga vyema katika masomo huku wengine wakisema
kuwa walikaa nyumbani ili kuepuka kuenea kwa janga la corona na sasa wamerejea
shule watasoma kwa bidii na watafaulu.
![]() |
Mwalimu Abubakari Shabani wa Shule ya Msingi Dodoma Mlimani anayefundisha Masomo ya Sayansi na Kingereza Darasa la saba katika shule hiyo |
Mwalimu
Abubakari Shaban ni mwalimu wa Darasa la Saba kwa somo la sayansi na kingereza
yeye alisema kuwa wamejipanga vizuri katika kufuata miongozo mbalimbali
iliyotolewa ikiwemo kuongeza muda wa masomo.
‘’kwenye
kuongeza muda wa mosomo na vipindi viteongezeka na sisi tutaenda kwa kasi ili
kuziba lile gepu ,na tutajitahidi kwenda kwa kasi ili kufanya wanafunzi waweze
kuelewa ili kwa yale madara ya mitihani waendelee kujiandaa vizuri na mitihani
yao ‘’Alisema Shaban
‘’Mikusanyiko
ilikataliwa kama unavyojua ufundishaji wetu wanafunzi ni lazima waje shueleni
sasa baada ya kufunga ikawa kuwapata wanafunzi ni changamoto kubwa,licha ya
kuwa kuna vipindi vilikuwa redioni na kwenye Runinga ilikuwa bado ni changamoto
kwa zile familia ambazo hazina uwezo huo ’’ Alisema Shaban
![]() |
Mwalimu Happines Sumaye anayefundisha Darasa la Nne katika shule hiyo akielezea furaha yake baada ya kurejea Shuleni |
Kwa
upande wake Mwalimu Happines Sumaye anayefundisha Darasa la nne katika shule
hiyo amesema anajisikia furaha kwa kurejea shuleni kwasababu ni kazi ambayo
wanaipenda.
‘’tunapenda
kuona jamii iliyo elimika , iliyostaarabika kwa hiyo kwa kipindi ambacho
hatukuwa shuleni kutokana na janga hili,tuliokuwa tunaona kabisa taifa letu
linavyokwenda kuporomoka lakini tunamshukuru Mungu hali imerejea kuwa nzuri,
watoto wamerejea shuleni wote wana afya nzuri ,tunamshukuru Mungu tunaendelea
na kazi’’ Alisema Sumaye
Dodoma
News Blog ilizungumzana Mwalimu Mkuu wa
Shule Teonila Mgulunde alisema anafurahi sana kufunguliwa kwa shule kwani kwa
kipindi cha miezi mitatu wanafunzi kukosa masomo ni ngumu mno na imewaumiza kwa
kiasi kikubwa.
![]() |
Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Dodoma Mlimani Teonila Mgulunde |
‘’Tunaishukukuru
sana serikali kwa uamuzi wake huu ,kwani idadi ya watoto waliorudi shuleni ni
wengi licha ya kuwa kuna mmoja tumempoteza lakini hakuuumwa ugonjwa huu alikuwa
na matatizo mengine lakini anamini kuwa baada ya kurejea shuleni malengo
yatatimia kwasababu tumeongezewa masaa ya vipindi kuzalishwa vipindi katika
masaa mawili ndivyo tulivyoambiwa kwenye muongozi ambao ulitolewa’’ Alisema
Mgulunde
Akizungumzia
kwa Madara ya mitihani alisema kuwa masaa mawili ambayo yaliongezwa yanawahusu
kama kawaida kwani katika shule yao wameshamaliza mada tangu mwezi wa tatu.
‘’kwahiyo
tuko katika marudio watoto wataendelea kufanya mitihani siku ya jumatano na
siku ya jumamosi na tutafanya tathimini mtihani wa jumamosi kwahiyo
tukishafanya tathimini lazima jumatano tufanyishe tena mtihani mwingine mpaka
siku ya mtihani wa Taifa hapo ni kwa darasa la saba lakini kwa upande wa Darasa
la nne wataendela kufanya mtihani siku ya jumamosi’’ Alisema Mgulunde
Hatahivyo
alisema kutokana muda wa vipindi kuongezwa amewasihi wazazi kuhakikisha kuwa mtoto
anapotoka nyumbani anakula vizuri lakini kwa wanaohitajika kuvaa barakoa wazazi
pia wanapaswa kuwahimiza watoto kuvaa barakoa kwani wapo watoto ambao hawai
kutokana na sababu za kiafya.
Tanzania
ni Miongoni mwa nchi chache ambazo zimefungua milango kwa wanafunzi kurudi
shule baada ya serikali kujiridhisha kupungua kwa maambukizi ya Covid-19 huku
ikisisitiza tahadhari kuendelea kuchukuliwa.
Mwisho.
Comments
Post a Comment