RC MAKONDA AZIDI KUWANYIMA USINGIZI WAPINZANI DAR, AKABIDHI MIRADI ILIYOTEKELEZWA NA SERIKALI YA RAIS MAGUFULI KUPITIA ILANI YA CCM


Na. Mwandishi Wetu,
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Mhe. Paul Makonda leo ameendelea na ziara yake ya kukabidhi miradi Mbalimbali iliyotekelezwa na serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais, Dkt. John Magufuli kwa Chama cha Mapinduzi CCM na kuwahimiza Wananchi kuchagua Viongozi wanaoweza kutatua kero zao.

Miongoni mwa Miradi aliyoikabidhi RC Makonda iliyotekelezwa kupitia Ilani ya CCM kwa upande wa Jimbo la Kinondoni ni Mradi wa Soko la Magomeni lenye thamani ya Shilingi Bilioni 8.9, Ujenzi wa Jengo la Mama na Mtoto hospitali ya Mwananyamala inayogharimu Bilioni 3 na Mradi wa Ujenzi wa Kiwanja Cha Mpira Mwenge chenye thamani ya Shilingi Bilioni 4.5.

Aidha, RC Makonda pia amekabidhi Mradi wa Ujenzi Barabara ya Morocco hadi Mwenge yenye thamani ya Bilioni 69.7, Mradi wa Kituo cha Mabasi Mwenge Bilioni 2.5 na Kituo cha Afya Kigogo chenye thamani ya Shilingi Bilioni 1.5.

Kesho Jumatano RC Makonda ataendelea na ziara yake kwenye Jimbo la Kibamba ambapo atakabidhi miradi mbalimbali ya maendeleo kwa Chama cha Mapinduzi CCM.

MWISHO

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.