CHUO KIMETENGA FUNGU MAALUMU KWAAJILI YA KUWASAIDIA WANATAALUMA WACHANGA WANAOCHIPUKIA-MWAKALOBO

Rasi wa Ndai ya Taaluma za Biashara na Sheria Chuo Kikuu cha Dodoma UDOM Adam Mwakalobo



Na Jackline Kuwanda, Dodoma.

Rasi wa Ndaki ya Taaluma za Biashara na Sheria Chuo kikuu cha Dodoma UDOM Adam Mwakalobo amefungua Warsha ya Mafunzo ya uhuru wa kujieleza kwa wanataaluma  wa ndaki ya Taaluma ya Biashara na Sheria Chuoni humo.

Akizungumza leo na Waandishi wa Habari mara baada ya kufungua mafunzo hayo amesema mafunzo yatakuwa ni endelevu kwasababu mwalimu muda wote anapaswa kupata mbinu mpya na vitu vipya kwani kila siku kumekuwa na mabadiliko mapya .

‘’unajua mabadiliko kila siku yanabadilika na kunavitu ambavyo vinaingia kwahiyo ni lazima tupate mbinu mpya za  kufundisha na kujifunza huwezi kukaa tu muda wote lazima upate vitu vipya na uongeze ujuzi kila wakati kwasababu ya haya mabadiliko yanayoendelea ndiyo maana ya haya mafunzo ‘’Mwakalobo

Amezungumzia pia kwa upande tafiti ambapo amesema  kuwa chuo kimetenga fungu maalumu kwaajili ya kuweza kuwasaidia wanataaluma wachanga wanaochipukia.

‘’ Chuo kinawasadia wanataaluma wachanga waweze kuomba zile hela yaani ni mashindano na wakipata wanaenda kufanya tafiti mbalimbali kulingana na maeneo yao ingawa sio kitu kikubwa sana lakini ni kuwawezesha ili waweze kujiendeleza ,kwasababu unajua kuandika machapisho na kwenda kushindana ni lazima uwe umejifunza  namna ya kuandika andiko’’Mwakaobo

Daktari Ines Kajiru ni Mkuu wa Idara ya Sheria Chuo Kikuu cha Dodoma UDOM amesema sio mara ya kwanza kufanya mafunzo kama hayo wamekuwa wakifanya mafunzo mbalimbali ikiwemo masuala ya kisheria huku akizungumzia kwa upande wa wanafaika wa mafunzo hayo .

‘’watu ni wengi wanaonufaika katika mafunzo kama haya nitolee mfano hapa leo watakao nufaika ni walimu wanataaluma wote wa ndaki ya Taaluma za Biashara na sheria wa chuo kikuu  cha Dodoma’’Kajiru

‘’ Tunacholenga ni kuendelea kukuza uelewa na kuwasaidia wanataaluma kuwajengea uwezo zaidi wa mambo mbalimbali kuhusu elimu na vilevile uhuru wa kujieleza na uhuru wa elimu’’ Kajiri

Mwalimu Idara ya Sheria Chuo cha Dodoma UDOM Nicodemas Husena

Naye mwalimu katika Idara ya Sheria  chuoni humo Nicodemas Husena amesema mafunzo kama hayo yanaongeza uelewa juu ya dhana nzima ya uhuru wa kujieleza.

‘’kwasababu kisheria ukisema uhuru wa kujieleza kuna mipaka, kuna haki unavitu huwezi kusema licha ya kuwa unauhuru wa kujieleza ,lakini vilevile kunavitu unaweza ukavisema lakini kwa mipaka fulani’’

‘’kwa mfano sisi Tanzania tuna sheria ya takwimu ambayo inazuia baadhi ya mambo kwahiyo mafunzo kama haya yanawafundisha washiriki wajue mipaka ya uhuru wa kujieleza lakini wajue ni yapi ambayo yanaweza yakazuiwa ‘’

Mafunzo hayo yamefanyika kwa ushirikiano wa Umoja wa Vituo vinavyotoa msaada wa kisheria wa vyuo vikuu Afrika Mashariki.

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.