YALIYOJIRI LEO MEI 30, 2020 WAKATI RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA DKT. JOHN POMBE MAGUFULI AKIWAKABIDHI NDEGE AINA YA TAUSI MARAIS WASTAAFU PAMOJA NA KUWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA OFISI ZA IKULU CHAMWINO, DODOMA
HAFLA YA MAKABIDHIANO YA NDEGE AINA YA TAUS*
#Rais Dkt. John Pombe Magufuli alipoingia
madarakani alikuta ndege aina ya tausi 403, hadi sasa wameongezeka na kufikia
2260. Tausi hao pia wamepelekwa katika Ikulu za mikoani, takriban tausi 540
wako katika Ikulu ya Dodoma.
#Rais Dkt. John Pombe Magufuli amewakabidhi
kila mmoja Hati na ndege 25 aina ya Tausi kwa Mjane wa Hayati Baba wa Taifa
pamoja na Marais Wastaafu watatu.
#Ugawaji wa ndege hawa kwa Mjane wa Hayati
Baba wa Taifa na Marais Wastaafu ni tukio kubwa na la kwanza hivyo napendekeza
itokee siku na wewe uridhie ili tukukabidhi na wewe Rais Dkt. Magufuli ndege
hawa kabla ya kustaafu - Katibu Kiongozi, Balozi John Kijazi.
#Tukio hili linaashiria kuwa pamoja na
viongozi kustaafu lakini bado mpo pamoja na Serikali - Balozi, John Kijazi.
#Nawashkuru Marais Wastaafu kwa kukubali kuja
kuchukua ndege hawa. Ndege hawa wana historia, Tanzania hatukuwahi kuwa na
Tausi bali waliletwa na Hayati Baba wa Taifa katika kipindi cha utawala wake
lakini wametunzwa vizuri na Marais Wataafu - Rais Dkt. John Pombe Magufuli.
#Hayati Baba wa Taifa aliwapenda hawa ndege
hivyo nimeona nitoe ndege hawa wakakae Butiama hata watu wanaoenda kutalii pale
wakafahamu kuwa haya ni matokeo ya upendo na busara yake kwa Watanzania, pia
wazee hawa waliwapenda na kuwatunza ndege vizuri ndio maana nimefanya uamuzi
huo - Rais Dkt. John Pombe Magufuli.
#Nakushkuru umefanya jambo kubwa kwa ajili
yetu, tumefurahi sana pia nakupongeza kwa maendeleo makubwa yanaondelea hapa
katika Ikulu hii - Rais Mstaafu, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete.
HAFLA YA UWEKAJI JIWE LA MSINGI UJENZI WA OFISI ZA IKULU CHAMWINO DODOMA
#Eneo la Ikulu ya Dodoma lina zaidi ya hekari
8473 ambapo limezungushiwa ukuta wenye urefu wa KM 27. Kwa ukubwa wa eneo hili
linaifanya Ikulu ya Tanzania kuwa ni moja ya Ikulu kubwa Duniani.
#Rais Dkt. John Pombe Magufuli ameendelea
kuweka wanyama mbalimbali katika Ikulu hii ambapo kwa kasi hii ya kuongezeka
kwa wanyama yapo mawazo ya kupafanya pawe na hifadhi ya wanyama ili watalii
waje kutembelea na kuongeza pato katika nchi yetu.
*Aliyosema Rais DKt. John Pombe Magufuli*
#Kutokana na umuhimu wa jengo hili la Ikulu,
sikuona umuhimu wa kufanya jambo hili peke yangu ndio maana nikawaomba Marais
Wastaafu tuje tushirikiane pamoja kuweka jiwe hili la msingi.
#Mnamo Oktoba 10,1973 Hayati Baba wa Taifa
alitangaza uamuzi wake wa kuhamishia Ikulu jijini Dodoma lakini pamoja na
kujengwa kwa makazi ya Rais nilipoingia madarakani niliahidi kuhakikisha
Serikali inahamia Dodoma.
#Pamoja na ujenzi unaoendelea, tayari majengo
matatu ya awali na ujenzi wa ukuta unaozunguka Ikulu vimeshakamilika. Aidha,
hakuna hata jengo moja la zamani litakalobomolewa.
#Nawapongeza jumla ya vijana 2400
waliogawanyika katika makundi mbalimbali pamoja na viongozi wenu kwa kufanya
kazi ya ujenzi wa Ikulu hii kwa ubora, endeleeni kuchapa kazi.
#Nimewaagiza Wizara ya Fedha na Mipango kutoa
jumla ya Sh. Bil. 2 kwa Jeshi la Kujenga Taifa ili kuhakikisha ujenzi wa Ikulu
hiyo unakamilika.
#Katika ugonjwa huu wa Corona Mungu
ametusaidia tumeshinda, Tanzania tuko salama.
#Ninaomba wakulima tujihadhari na kuuza mazao
yetu kwa bei ya chini, mwaka huu umekua mzuri kwani tutapata chakula cha
kutosha hivyo kama kuuza tuuze katika muda muafaka, hapo ndipo tutapata faida
ya mazao yetu.
#Hivi sasa Dodoma imeshakua, mbali ya kujenga
ofisi za Serikali na kufanikiwa kuwahamisha watumishi, Serikali imeendelea
kuimarisha miundombinu na kuboresha huduma za jamii.
#Tayari tumejenga barabara nyingi za lami na
nyingine zinaendelea kujengwa ikiwemo barabara yenye KM 51 kwenye Mji wa
Serikali pia tupo kwenye hatua za mwisho za kumpata Mkandarasi wa kujenga
barabara ya mzunguko ya njia nne yenye urefu wa KM 110.
#Tumepanua uwanja wa ndege wa Dodoma, taratibu
za kumpata Mkandarasi kwa ajili ya ujenzi wa uwanja mpya mkubwa wa ndege wa
msalato mchakato unaendelea.
#Tumekamilisha ujenzi wa stendi kuu ya mabasi
kwa gharama ya sh. Bil.24.033 pamoja na soko kuu litakalogharimu sh. Bil.14.649
na kwa upande wa huduma za maji kwa sasa tunaendelea na maandalizi ya ujenzi wa
bwawa ambalo litazalisha lita 128,000 kwa siku na umeme upo wa kutosha, kuna
ziada ya MW 21 hapa Dodoma.
*Aliyosema Rais Mstaafu, Ali Hassan
Mwinyi.*
#Ningependa kujiunga na wenzangu kutoa pongezi
maalum kwa mwenyeji wetu ambaye ni kijana kuliko mimi na ni chanzo chema cha
fikra na maendeleo na nina uhakika wote tumefurahi kuona namna anavyoliongoza
taifa letu, kwa namna mpya na nzuri. Natoa shuk rani na pongezi za hadharani.
*Aliyosema Rais Mstaafu, Benjamin William
Mkapa.*
#Tunashukuru kwa kukumbukwa na kupewa zawadi
ya ndege hawa tulio watunza kwa miaka yote 30. Tunakushukuru kwa uaminifu wako
kwa Chama na Serikali uliyoiunda. Uamuzi wa Serikali kuhamia Dodoma ni jitihada
za muda mrefu na kila awamu ilifanya jitihada. Rais Magufuli amefanya mengi
zaidi na sasa Serikali imehamia Dodoma. Nasisitiza, Mbele kwa mbele, endelea
hivyo!
*Aliyosema Rais Mstaafu, Dkt. Jakaya Mrisho
Kikwete.*
#Mwaka 1971 Chama cha Tanu kiliamua Makao
Makuu ya Nchi yahamie Dodoma, na ni uamuzi uliofanywa kidemokrasia, Mikoa
ilitoa maoni na mingi ilikubali kasoro Mkoa wa Pwani. Ulikua ni uamuzi
shirikishi na sio mawazo ya Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere pekee .
#Rais Magufuli nakupongeza sana kwa uamuzi wa
busara na wa hekima wa kujenga IKULU, Hapa ndio kilele chenyewe. Naungana na
wenzangu kukupongeza na kukuombea uhai ushiriki katika kukata utepe baada ya
ujenzi huu kukamilika.
*Aliyosema Katibu Mkuu Ikulu, Moses Kusilo.*
#Mnamo mwaka 2017 shughuli mbalimbali za
ujenzi wa majengo mapya, ujenzi wa barabara na ujenzi wa ukuta pamoja na
ukarabati wa majengo yaliyokuwepo.
#Rais Dkt. John Pombe Magufuli mnamo Januari
2020, alielekeza kuanza kwa ujenzi katika eneo hili na kusisitiza kuwa usanifu
wa majengo hayo ufanane kabisa na Ikulu ya Dar es Salaam, alisisitiza kuwa
ujenzi huo ufanywe na wazalendo wa hapa hapa nchini.
*Aliyosema Mkuu wa JKT, Brigedia Genarali,
Charles Mbuge.*
#Jeshi la kujenga Taifa lilikabidhiwa eneo la
Chamwino lenye ukubwa wa mita za mraba 9340 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa ofisi
ya Rais na jengo la utawala mnamo Februari, 2020, ujenzi unaendelea na fedha
iliyotolewa hadi sasa ni sh. Bil.1.
#Jeshi la kujenga Taifa limeendelea kuchukua
tahadhari za kujikinga na ugonjwa wa Corona, tunaendelea kutengeneza barakoa,
vitakasa mikono na vifaa kinga na kuviuza kwa wananchi kwa bei rahisi.
IMEANDALIWA NA IDARA YA HABARI - MAELEZO
Comments
Post a Comment