Wananchi mkoani Njombe wamjia juu mtendaji wa kijiji kwa kuuza eneo lililotengwa kwaajili ya ufugaji wa kilimo


Na. Mwandishi Wetu, NJOMBE
Wananchi wa vijiji vya kata ya Itulahumba halmashauri ya wilaya ya wangingombe mkoani Nombe kwa pamoja wamepinga kitendo kinachofanywa na baadhi ya wananchi wenzao kwa kushirikiana na mtendaji wa kijiji hicho cha kuuza eneo ambalo limetengwa kijijini hapo kwaajili ya ufugaji na kilimo.

Eneo hilo lenye ukubwa wa zaidi ekari 80 ambalo limeanza kukatwa miti na kulimwa bila makubaliano ya kamati za vijiji pamoja na mkutano wa hadhara wa wananchi
hao akiwemo Yohana Mgute na Mary Mwakajuba wamesema serikali isaidie waliovamia kukamatwa na kuzuia uharibifu unaoendelea.

Mtendaji wa kijiji hicho Rudlof Mbilo anasema eneo hilo licha ya kuwa limetengwa kwajili ya shughuli za kilimo na ufugaji lakini hakuna nyaraka zinazothibitisha na ndio sababu amekuwa akiidhinisha watu kuuziana ardhi hiyo.

viongozi wa kata hiyo wakiongozwa na Diwani, Thobias Mkane na Betty Mangula Afisa Mtendaji wa Kata Hiyo wamepiga marufuku   mtu yeyote kufanya shughuli katika eneo hilo wakati uchunguzi wa kuwabaini waliovamia na kuuza ukiendelea.

MWISHO



Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.