WAKUU WA VYUO WATAKIWA KUTOKUINGILIA UHURU WA IBADA


Na. Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM

Wakuu wa vyuo pamoja na shule nchini wametakiwa kutokuingilia uhuru wa kufanya ibada kwa wanafunzi pindi ambapo wanarejea mashuleni baada ya kupungua kwa kasi ya maambukizi ya virusi vya Corona.

Hayo yameelezwa na Kiongozi Mkuu wa Kanisa la Waadventista wasabato, Jimbo Kuu la Kusini mwa Tanzania, Askofu Mark Maleleana wakati akikabidhi vifaa kinga kwa hospital za Wilaya ya Temeke ili kupambana na maambukizi ya virusi vya Corona.

Askofu Malekela amesema kuwa nchi imefikia hapa kutokana na maombi yaliyoongozwa na Rais Magufuli hivyo wanafunzi wapatiwe muda wa kufanya ibada.

Akipokea msaada huo kwa niaba ya Mganga Mkuu wa hospitali ya Temeke, Bi. Grace Ntangu amesema kuwa vifaa kinga hivyo vitatumika kwa makususi yaliyokusudiwa.

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.